Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/04 uku. 5
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 4/04 uku. 5

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Toa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho au matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawashirikiani na tengenezo, jitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Jitahidi sana kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa na watu ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Watu fulani wakisema kwamba hawana watoto, watolee broshua Anataka. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ukitumia broshua hiyo. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua zifuatazo zinaweza kutolewa katika maeneo fulani inapofaa: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them.

◼ Kuanzia Juni, beji za kusanyiko la wilaya la 2004 zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo wa kutaniko. Beji zitapakiwa kwa mafungu ya kadi 25 ikitegemea ukubwa wa kutaniko. Ikiwa kutaniko linahitaji beji zaidi, zapasa kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Vifuko vya beji vya plastiki vyaweza kuagizwa kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevitaka.

◼ Ni lazima ofisi ya tawi iwe na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) na kuituma kwa ofisi ya tawi haraka iwezekanavyo. Fomu hiyo yapasa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika namba ya simu ya eneo lao.

◼ Waandishi wa kutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Fomu hizo zaweza kuagizwa kupitia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni angalau akiba ya mwaka mmoja. Chunguzeni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa vizuri, kutia ndani na tarehe ya ubatizo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki