Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Julai 12
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15 na Amkeni! la Juni 22. Katika onyesho moja, mhubiri amtolee gazeti mtu aliye barabarani ambaye anaongea lugha tofauti.
Dak. 18: “Iga Haki ya Yehova.”a Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Dak. 15: Biblia—Kitabu cha Matabiri Yanayotegemeka. Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa 27-29. Katika huduma yetu, mara nyingi sisi hukutana na watu wanaopendezwa na wakati ujao. Biblia huandaa habari inayotegemeka inayoonyesha wakati ujao ulio mzuri kwa ajili ya wanadamu watiifu. Zungumzia baadhi ya unabii wa Biblia unaoimarisha uhakika katika utabiri wa wakati ujao wa Biblia. Panga mhubiri atoe onyesho fupi kuhusu jinsi matukio ya Biblia yanavyoweza kutumiwa kumsaidia mtu anayependezwa aimarishe uhakika katika Biblia.
Wimbo 16 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia umuhimu wa kudumisha programu ya kawaida ya kusoma Biblia kila siku, hata wakati mambo mengine yanapovuruga utaratibu wetu. Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 2000, ukurasa wa 32.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 1.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Ruhusu wasikilizaji watoe maelezo kuhusu habari katika kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 572-574, inayoonyesha maendeleo ya kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia nyakati zetu. Chochea upendezi kwa ajili ya mfululizo wa makala zinazokuja. Baadhi ya vichwa vitakavyozungumziwa ni vile vinavyohusu jinsi ya kutayarisha na kuongoza funzo, jinsi ya kumsaidia mwanafunzi kutayarisha, kiasi cha habari za kujifunza, jinsi ya kutumia maandiko kwa matokeo, jinsi ya kujibu maswali ya mwanafunzi, jinsi ya kuanzisha sala, na jinsi ya kumwelekeza mwanafunzi kwenye tengenezo. Watie wote moyo watumie madokezo yaliyopo na kuweka makala hizo kwa ajili ya kurejelea baadaye.
Wimbo 10 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 26
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1 na Amkeni! la Julai 8. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Mbona ninyi mnatembelea watu mara nyingi mno?”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 20.
Dak. 8: Sanduku la Swali. Ishughulikiwe na mzee. Soma na kuzungumzia makala nzima.
Dak. 25: “Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la Biashara.”b Taja mipango ya kwenu ya kuhubiri eneo la biashara. Toa maonyesho mawili mafupi ya utoaji ulio katika fungu la 4-5 au utoaji mwingine ambao umekuwa na matokeo kwenu. Muda ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe mambo mazuri yaliyoonwa waliyopata wakihubiri katika eneo la biashara.
Wimbo 173 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 2
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 22: Je, Wewe Hutoa Sababu? Hotuba na mazungumzo yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 254, fungu la 1-2. Tunapofafanua na kutumia maandiko katika huduma ya shambani na kutoka jukwaani, ufundishaji wetu utakuwa na matokeo zaidi tukitoa sababu kwa ajili ya yale tunayosema badala ya kusisitiza tu mambo. Ukitumia mifano kutoka katika kitabu Kutoa Sababu au vingine ambavyo vinafaa eneo lenu, onyesha jinsi ya (1) kuteua na kufafanua mambo makuu katika andiko, (2) kutoa uthibitisho unaounga mkono kutoka kwenye muktadha au kutoka katika andiko lingine linaloshughulikia habari hiyo, (3) kutumia mfano ili kuonyesha sababu ya yale ambayo umesema, na (4) kutumia maswali ili kuwasaidia wasikilizaji wafikirie habari hiyo. Kazia faida za kutumia njia ya kutoa sababu.
Dak. 15: Tumia vema Kitabu cha Mwaka cha 2004. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Taja mambo makuu ya “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza,” tarakimu zenye kutokeza kutoka kwenye ripoti ya ulimwenguni pote, na mambo machache yaliyoonwa yanayoimarisha imani. Watie moyo wote wakisome kitabu kizima mwaka huu.
Wimbo 32 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.