Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 7
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 7

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Agosti 30, 2004. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa kuanzia juma la Julai 5 hadi Agosti 30, 2004. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunawezaje kueleza sababu ya tumaini letu “kwa tabia-pole na heshima kubwa”? (1 Pet. 3:15) [be uku. 192 fu. 2-4]

2. Kwa nini ni muhimu kuzungumza kwa usadikisho? (Rom. 8:38, 39; 1 The. 1:5; 1 Pet. 5:12) [be uku. 194]

3. Tunawezaje kuonyesha usadikisho? [be uku. 195 fu. 3–uku. 196 fu. 4]

4. Busara ni nini, kwa nini ni muhimu, na tunawezaje kuwa wenye busara lakini thabiti? (Rom. 12:18) [be uku. 197]

5. Mtu mwenye busara atafikiria nini kabla ya kuzungumza? (Met. 25:11; Yoh. 16:12) [be uku. 199]

HOTUBA NA. 1

6. Mazungumzo yetu na mazoea yetu ya kujifunza yanawezaje kuonyesha maendeleo ambayo tumefanya katika kweli? [be uku. 74 fu. 3–uku. 75 fu. 2]

7. Inamaanisha nini ‘kujinunulia wakati unaofaa,’ na tunawezaje kufanya hivyo? (Efe. 5:16) [w02 11/15 uku. 23]

8. Maandiko yanaonyeshaje wazi kwamba wanadamu wote ni sawa mbele za Mungu, na jambo hilo linapaswa kuathirije huduma yetu? [w02 1/1 uku. 5, 7]

9. Yehova, jina la kipekee la Muumba, linamaanisha nini? [w02 1/15 uku. 5]

10. Ni nini kilichofanya dhabihu ya Abeli iwe “ya thamani kubwa zaidi” kuliko ya Kaini, na jambo hilo linatufunza nini kuhusu ‘dhabihu yetu ya sifa’? (Ebr. 11:4; 13:15) [w02 1/15 uku. 21 fu. 6-8]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Andiko la Mambo ya Walawi 18:3 linawezaje kutusaidia kuepuka viwango vilivyopotoka vya kuamua mema na mabaya? (Efe. 4:17-19) [w02 2/1 uku. 29]

12. Ni nini kilichofananishwa na “mikate miwili” iliyotolewa na kuhani mkuu kuwa “toleo la kutikisa” wakati wa Sherehe ya Majuma (Pentekoste)? (Law. 23:15-17) [w98 3/1 uku. 13 fu. 21]

13. Katika kisa cha uzinzi kama kile kinachotajwa katika Hesabu sura ya 5, ni katika maana gani “paja” la mwanamke mzinifu ‘lingeanguka’? (Hes. 5:27) [w84-SW 10/15 uku. 23 au w84-E 4/15 uku. 29]

14. Kwa nini Miriamu na Haruni walimshutumu Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi? (Hes. 12:1)

15. “Kitabu cha Vita vya Yehova” kilikuwa nini? (Hes. 21:14)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki