Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Septemba: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Pia unaweza kutoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? (kikubwa au kidogo) badala yake, au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Oktoba: Nakala mojamoja za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! zitatolewa mwezi wote. Habari zaidi zitatolewa baadaye ili kuhakikisha kwamba ugavi wa kawaida wa magazeti umetumiwa wote. Mahali ambapo kuna mtu anayependezwa, tafadhali toa broshua Anataka, na ufuatie ukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Watu wakisema kwamba hawana watoto, toa broshua Anataka. Tia bidii kutumia broshua hiyo ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko kabla ya Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya 2005, Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2005, na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2005 katika ombi lao la vichapo litakalofuata. Orodha ya lugha ambazo vichapo hivyo vinapatikana itakuwa katika barua kwa makutaniko yote.