Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 13
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ikiwa mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 yanafaa eneo la kutaniko lenu, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 15 na Amkeni! la Agosti 22. Utoaji mwingine unaweza kutumiwa. Baada ya kila onyesho, kazia kwa ufupi jambo muhimu katika onyesho hilo.
Dak. 15: “Uwe na Jicho Rahisi.”a Tumia maswali yaliyopo. Kazia maandiko yaliyotajwa kadiri wakati unavyoruhusu.
Dak. 18: Wanashuhudia Matendo Yetu Mazuri. (1 Pet. 2:12) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2002, ukurasa wa 12-14, fungu la 14-20. Waombe wasikilizaji wasimulie jinsi ambavyo watu wa eneo lenu wamevutiwa kwa sababu ya kuona matendo yetu mazuri.
Wimbo 162 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu ya barua kutoka ofisi ya tawi, iliyo kwenye ukurasa wa kwanza wa toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme. Watie moyo wote wasome Hesabu 16:1-35 kisha watazame vidio Respect Jehovah’s Authority, ikiwa inapatikana, wanapojitayarisha kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 4.
Dak. 15: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba itolewe na mzee ikitegemea ripoti ya utumishi ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2004. Kazia mambo yenye kutia moyo katika ripoti hiyo, na ulipongeze kutaniko kwa ajili ya mambo mazuri waliyotimiza. Kazia jitihada za mapainia. Taja jambo moja au mawili ambayo kutaniko linaweza kufanyia kazi mwaka ujao.
Dak. 20: Kuvumilia Katika Kazi Zilizo Njema. (Gal. 6:10) Wahoji wahubiri wawili au watatu ambao ni mapainia wa kawaida au ambao hufanya upainia msaidizi mara kwa mara. Wamekabili magumu gani katika utumishi wao kwa Yehova, na wameyashindaje? Ni nini kimewasaidia kuvumilia wanapowatendea wengine mema? Jitihada zao katika huduma ya Kikristo zimewafaidije wao na wengine? Ikiwa inafaa, eleza pia jitihada ambazo mmefanya kwenu ili kuwahubiria habari njema watu wanaozungumza lugha nyingine. Wapongeze wote kwa ajili ya ‘kazi yao ya uaminifu na kazi yao ya jasho yenye upendo na uvumilivu wao.’—1 Thes. 1:2, 3.
Wimbo 103 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 27
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Septemba. Panga onyesho la kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1 na Amkeni! la Septemba 8.
Dak. 10: Neno la Yehova Liko Hai. Hotuba. Ili kutusaidia tufaidike kikamili na programu ya usomaji wa Biblia wa kila juma katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mfululizo wa makala zenye kichwa “Neno la Yehova Liko Hai” zimeanza kuchapishwa katika matoleo fulani ya Mnara wa Mlinzi. Ukitumia Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 2004, ukurasa wa 24-27, taja sehemu mbalimbali za makala hizo. Baada ya kutoa muhtasari, sehemu yenye kichwa “Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa” inaeleza baadhi ya mistari migumu ya Kimaandiko. Sehemu yenye kichwa “Mambo Tunayojifunza” hutusaidia kuelewa umuhimu wa habari tuliyosoma. Zungumzia mifano michache hususa ili kuonyesha jinsi mfululizo huo utakavyotusaidia kuelewa kindani Neno la Mungu. Watie moyo wote watumie kikamili makala hizo mpya tunapoanza kusoma kitabu cha Kumbukumbu la Torati wiki ijayo.
Dak. 20: “Itumie Biblia Vizuri.”b Tumia maswali yaliyopo. Utangulizi unapaswa kutegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 145, fungu la 2-3. Tia ndani maonyesho mawili mafupi, moja likiwa ziara ya kwanza na la pili likiwa ziara ya kurudia. Yanapaswa kuonyesha jinsi ya kutumia mapendekezo yaliyotolewa.
Wimbo 38 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 4
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Ona pia ukurasa wa 4.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji.
Dak. 25: Tii kwa Uaminifu Mamlaka ya Kimungu. Hotuba itolewe na mwangalizi msimamizi ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 2002, ukurasa wa 9-14. Zungumza na wasikilizaji jinsi Kora na wafuasi wake walivyokosa kuonyesha ushikamanifu kuhusiana na mambo sita mbalimbali. Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 2002, ukurasa wa 29, fungu la 1. Au, ikiwa vidio inapatikana, zungumzieni makala “Lazima Tuheshimu Mamlaka ya Yehova.” Soma Yuda 11, utangulizi usizidi dakika mbili. Kisha anza moja kwa moja mazungumzo pamoja na wasikilizaji ukitumia maswali yote yaliyo katika makala hiyo. Kazia kwamba ili tuendelee kuwa na kibali cha Yehova, ni lazima tuepuka mtazamo wa uasi wa Kora na kuiga mfano wa wanawe, ambao hawakuruhusu chochote kivunje uaminifu wao kwa Yehova.
Wimbo 99 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.