Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Septemba: Je, Kuna Muumba Anayekujali? Au mnaweza kutoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? (chapa kubwa au ndogo), au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatatolewa mwezi mzima. Habari zaidi zitatolewa baadaye ili kuhakikisha kwamba magazeti yanayopokewa kwa ukawaida yanatumiwa. Mtu anapopendezwa, tafadhali anza mazungumzo katika broshua Anataka, kisha umrudie ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mtu akisema kwamba hana watoto, toa broshua Anataka. Jitahidi kutumia broshua hiyo kuanzisha mafunzo ya Biblia. Desemba: Toa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. La sivyo, toa vichapo vingine kama vile, Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
◼ Vidio yenye kichwa No Blood—Medicine Meets the Challenge itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi mwezi wa Desemba. Ikiwa mnahitaji nakala za kaseti hiyo ya vidio mnapaswa kuziagiza haraka iwezekanavyo kupitia kutaniko.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya 2005 itatolewa Jumapili, Aprili 10. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwisho-juma huo, yatakuwa na hotuba hiyo juma linalofuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Jumapili, Aprili 10, 2005.
◼ Kila Septemba, Halmashauri ya Uendeshaji wa Jumba la Ufalme inapaswa kujaza nakala mbili za Orodha ya Utunzaji/Ukaguzi wa Mambo ya Usalama wa Jumba la Ufalme (CN-14) na kutuma nakala moja kwenye Dawati la Ujenzi wa Majumba ya Ufalme katika ofisi ya tawi. Mwangalizi wa mzunguko atachunguza orodha hiyo anapotembelea kutaniko.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa 21-23 wa Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1991, kuhusu watu waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao wanapaswa kutembelewa.
◼ Makutaniko yanapaswa kuwapa wahubiri magazeti mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapofika. Hilo litawawezesha wahubiri kufahamu mambo yaliyomo kabla ya kuyatoa katika utumishi wa shambani.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Oktoba utakuwa na miisho-juma mitano, ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.