Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Novemba 1-14: Kampeni ya pekee ya kugawa broshua Endeleeni Kukesha! Novemba 15-30: Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mtu akisema kwamba hana watoto, toa broshua Anataka. Unapotumia broshua hiyo, jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Desemba: Toa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi au vichapo vingine kama vile, Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari 2005: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kwenye karatasi inayochujuka au kugeuka rangi na kuwa manjano au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya 1990 chaweza kutolewa, na pia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari 2005: Kitabu Mkaribie Yehova.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Desemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti ya benki ya kushughulikia udumishaji au ujenzi, fanyeni mipango ili kukagua hesabu hiyo pia. Kukaguliwa kwa hesabu kukikamilika, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya mwaka wa 2004 pamoja na ombi lifuatalo la vichapo. Hadi mabuku yaliyojalidiwa yapatikane na upakizi ufanywe, hayo yataonyeshwa chini ya “Zitatumwa Zikipatikana” katika orodha ya upakizi ya kutaniko. Mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za ombi la pekee.
◼ Kuanzia juma la Mei 23, 2005, tutajifunza broshua Endeleeni Kukesha! kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Ni lazima ofisi ya tawi iwe na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yapaswa kujaza fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) na kuituma kwenye ofisi ya tawi haraka iwezekanavyo. Fomu hiyo yapasa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika namba ya simu ya eneo lao.