Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/04 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Sifa ya Kiasi Bado Ni Muhimu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Unaweza Kudumisha Sifa ya Kiasi Unapojaribiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Kusitawisha Kiasi cha Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kiasi cha Kikristo Ni Uthibitisho wa Hekima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 11/04 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Tushughulikieje migawo ya kutaniko?

Ni lazima ndugu wafanye mambo kwa umoja ili kuwe na utaratibu katika kutaniko la watu wa Yehova. (1 Kor. 14:33, 40) Fikiria mambo yanayohitaji kutimizwa katika mkutano mmoja tu wa kutaniko. Mbali na programu yenyewe, ndugu na dada huwa na migawo mingi ya kushughulikia kabla na baada ya mikutano. Migawo mingine ambayo hushughulikiwa pasipo kuonekana ni muhimu pia. Sote tunawezaje kuunga mkono mpango huo?

Jitolee. Wale walio na roho ya kujitolea watakuwa na mengi ya kufanya. (Zab. 110:3) Onyesha kwamba unawajali wagonjwa na walio wazee. Saidia kusafisha Jumba la Ufalme. Tunaweza kufanya mambo mengi yenye manufaa bila kuombwa tujitolee. Tunahitaji tu kuwa na tamaa ya kusaidia.

Uwe mwenye kiasi unapotumikia. Watu wenye kiasi hufurahia kuwatumikia wengine. (Luka 9:48) Sifa ya kiasi itafanya tuepuke kukubali migawo mingi tusiyoweza kuishughulikia vizuri. Pia, tukiwa na kiasi tutaepuka kujitwika madaraka yasiyo yetu.—Met. 11:2.

Uwe mwenye kutegemeka. Musa alitiwa moyo achague “wanaume wenye kutegemeka” washughulikie madaraka fulani katika Israeli la kale. (Kut. 18:21) Sifa hiyo inahitajiwa leo. Shughulikia kila mgawo unaopewa kwa uangalifu. (Luka 16:10) Ikiwa huwezi kushughulikia mgawo fulani, hakikisha kwamba umefanya mipango ifaayo ili mtu mwingine aushughulikie.

Fanya yote uwezayo. Wakristo wanahimizwa wafanye kazi kwa nafsi yote, hata kazi za kimwili. (Kol. 3:22-24) Tuna sababu kubwa hasa ya kufanya hivyo tunapojitahidi kuendeleza ibada ya kweli. Hata mgawo uonekane kuwa wa hali ya chini, kutaniko linanufaika unapofanywa vizuri.

Kila mgawo hutupa fursa ya kuonyesha upendo wetu kwa Yehova na kwa ndugu zetu. (Mt. 22:37-39) Na tushughulikie migawo yetu mbalimbali kwa uaminifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki