Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu) ili kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15 na Amkeni! la Desemba 22. Maonyesho mengine yanayofaa yanaweza kutumiwa. Katika mojawapo ya maonyesho hayo mhubiri anamtolea magazeti mtu wa ukoo ambaye si Shahidi.
Dak. 15: “Tunalishwa Maneno ya Imani.”a Kwa kadiri wakati unavyoruhusu, soma na uzungumzie maandiko ambayo yametajwa.
Dak. 20: “Jaribu Kutumia Utangulizi Unaoweza Kubadilishwa Ufaane na Hali.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu ukurasa wa 6 wa nyongeza. Onyesha njia mbili za kutumia utangulizi huu, kichapo cha mwezi huu kinapotolewa. Katika kila onyesho, mhubiri asome andiko moja linalohusu hangaiko ambalo mwenye nyumba ametaja.
Wimbo 143 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Je, Vijana Mnafanya Maendeleo ya Kiroho? Hotuba hii itolewe na mzee ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 2003, ukurasa wa 8-10. Taja miradi ambayo inaweza kutimizwa, na uwatie vijana moyo wajiwekee miradi hususa ya kiroho.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 5.”b Panga onyesho linalohusu mhubiri stadi akizungumza na mhubiri mpya juu ya jinsi ya kuepuka mitego inayotajwa katika fungu la 4-5.
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia kifupi sanduku “DVD Yenye Sehemu Tatu.”
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba.
Dak. 25: “Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo”c Tumia maswali yaliyopo. Taja kwamba katika ukurasa wa 3-5 wa nyongeza ya mwezi huu kuna mapendekezo ya jinsi ya kutoa vichapo ambavyo ni toleo la miezi mbalimbali. Tunza nyongeza hiyo ili uweze kuitumia mwaka huu wote. Baada ya kuzungumzia makala, zungumzia jinsi tunavyoweza kuwatolea watu kitabu Mkaribie Yehova katika mwezi wa Februari. Panga kuwe na maonyesho mawili. Maonyesho hayo yanaweza kutegemea mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 3, au mapendekezo mengineyo yanayofaa eneo lenu.
Wimbo 200 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 31
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti ya utumishi ya mwezi wa Januari. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi wa Januari 1 au Amkeni! la Januari 8. Njia nyingine zinazofaa zinaweza kutumiwa.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Je, Unayachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2005. Ikiwa kitabu hicho hakijapatikana bado kutanikoni, tumia dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2004. Zungumzia umuhimu wa kutenga dakika chache kila siku ili kusoma andiko la siku na maelezo yake. Panga mapema ili ndugu au dada mmoja au wawili waeleze kuhusu mipango yao ya kusoma andiko la siku na jinsi ambavyo wamefaidika. Malizia kwa kuzungumzia kifupi andiko la mwaka la 2005.
Wimbo 184 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Wasaidie Wapya Wajifunze Kumpenda Mungu na Jirani. Hotuba inayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2004, ukurasa wa 16, fungu la 7-9. Kazia jinsi ambavyo kila mmoja kutanikoni anawasaidia wapya kuwa wanafunzi wa Kristo.
Dak. 20: Yehova Hawanyimi Watu Wake Kilicho Chema. (Zab. 84:11) Wahoji ndugu na dada kadhaa ambao wamevumilia majaribu kwa uaminifu. Wamekabili magumu gani? Ni nini kilichowasaidia wavumilie? Wamepata baraka gani?
Wimbo 104 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.