Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Februari 28, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa kwenye hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Januari 3 hadi Februari 28, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunawezaje kufanya usemi wetu ueleweke vizuri zaidi? [be uku. 226 fu. 1–uku. 227 fu. 1]
2. Ni maneno ya aina gani ambayo huenda ukahitaji kuyafafanua zaidi? [be uku. 227 fu. 2–uku. 228 fu. 1]
3. Ni mbinu gani ambayo itatusaidia kuzungumzia habari kwa njia inayowaelimisha wasikilizaji wetu vizuri? [be uku. 231 fu. 1-3]
4. Tunawezaje kueleza andiko ambalo wasikilizaji wanalijua kwa njia yenye kuwaelimisha? [be uku. 231 fu. 4-5]
5. Huenda kukawa na matokeo gani tukiwatia moyo wasikilizaji wetu wazingatie mambo madogo-madogo katika masimulizi ya Biblia ambayo wanayajua? [be uku. 232 fu. 2-4]
HOTUBA NA. 1
6. Ni nini kinachohusika katika kuwafunza watu ‘kumwogopa Mungu wa kweli na kushika amri zake’? (Mhu. 12:13) [be uku. 272 fu. 3–p. 273 fu. 1]
7. Tunawezaje kukazia jina la Yehova na pia sifa zake? (Yoe. 2:32) [be uku. 274 fu. 3-5]
8. Ni muhimu kadiri gani kujifunza juu ya Yesu na kutoa ushahidi kumhusu? (Yoh. 17:3) [be uku. 275 fu. 6]
9. Je, kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu na kuielewa Biblia kunahusianaje moja kwa moja na kuelewa daraka la Yesu? [be uku. 276 fu. 1]
10. Tunawezaje kuonyesha tunaamini kabisa kwamba Yesu Kristo ni Mfalme? [be uku. 277 fu. 4]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Je, Tera, baba ya Abrahamu, alikuwa mwabudu wa sanamu? (Yos. 24:2)
12. Je, Gideoni alikosa ujasiri wa kutimiza mgawo ambao Yehova alimpa? Kwa nini unajibu hivyo? (Amu. 6:25-27) [w00 8/1 uku. 17 fu. 12]
13. Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Gideoni alivyozungumza na kabila la Efraimu? (Amu. 8:1-3) [w00 8/15 uku. 25 fu. 3-4]
14. Watu wa Gibea walidhihirisha nini walipokataa kuwakaribisha wageni? (Amu. 19:14, 15)
15. Ikiwa “kila mmoja alikuwa na mazoea ya kufanya yaliyokuwa mema machoni pake mwenyewe,” je, jambo hilo lilisababisha mchafuko? (Amu. 21:25)