Matangazo
◼ Februari: Kitabu Mkaribie Yehova kitatolewa. Machi: Toa broshua Endeleeni Kukesha. Ikiwa mtu anapendezwa kikweli, mwonyeshe kitabu Ujuzi ukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia. Aprili na Mei: Toa gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho au pindi nyingine za kiroho lakini ambao hawahudhurii mikutano ya kutaniko, jitahidi kutoa kitabu Mwabudu Mungu. Lengo linapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia, hasa pamoja na wale ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu ya kutaniko Machi 1, au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti ya benki ya kushughulikia udumishaji au ujenzi wa Jumba la Ufalme, fanyeni mipango ili kukagua akaunti hiyo pia. Ukaguzi huo unapokamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa taarifa hiyo ripoti ya hesabu itakaposomwa.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa yeyote ana tatizo la kutimiza takwa la saa, wazee wanapaswa kupanga kumsaidia. Mapendekezo yanapatikana katika barua za kila mwaka za S-201-SW.
◼ Kichwa cha hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya 2005 kitakuwa “Kwa Nini Yesu Aliteseka na Kufa?” Ona tangazo linalohusu jambo hili kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2004.
◼ Wote wanapaswa kuhudhuria Mkutano wa Watu Wote, Jumapili, Machi 20, ili kusikiliza tangazo la pekee kuhusu mpango fulani ambao utaandaliwa kwa ajili ya wahubiri.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kupelekwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za ombi la pekee.