Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 kur. 3-5
  • Majira ya Ukumbusho Ni Wakati wa Kuongeza Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majira ya Ukumbusho Ni Wakati wa Kuongeza Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Ratiba za Painia-Msaidizi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 2/05 kur. 3-5

Majira ya Ukumbusho Ni Wakati wa Kuongeza Utumishi

1 Waisraeli wa kale waliadhimisha “sherehe za majira za Yehova” kila mwaka katika siku zilizowekwa. (Law. 23:2) Walipotenga wakati ili kutafakari wema wa Mungu, walifurahi sana na kusukumwa kuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi.—2 Nya. 30:21–31:2.

2 Siku hizi, tunaongeza utumishi wetu wenye shangwe wakati wa majira ya Ukumbusho ya kila mwaka. Huo ni wakati wa kufikiria kwa uzito zawadi yenye thamani kubwa ambayo Yehova alitoa kwa ajili yetu, yaani, Mwana wake mzaliwa-pekee. (Yoh. 3:16; 1 Pet. 1:18, 19) Tunapotafakari upendo ambao tumeonyeshwa na Mungu na Mwana wake, tunasukumwa kumsifu Yehova na kujitahidi kufanya mapenzi yake.—2 Kor. 5:14, 15.

3 Mwaka huu, Mlo wa Jioni wa Bwana utaadhimishwa Alhamisi, Machi 24, baada ya jua kushuka. Tunawezaje kuongeza utumishi katika mwezi wa Machi, Aprili, na Mei?

4 Kuwahubiria Watu Wengi Zaidi: Jitahidi kuwahubiria watu wengi iwezekanavyo unapokuwa katika utumishi wa shambani. Je, unaweza kupanga kwenda nyumba kwa nyumba wakati ambapo watu wengi wako nyumbani, kama vile saa za alasiri au jioni? Iwapo baadhi ya wahubiri katika funzo lenu la kitabu wangependa kwenda kuhubiri kabla ya funzo, mwangalizi wa funzo la kitabu anaweza kupanga mkutano mfupi wa utumishi ili kuhubiri kwenye eneo lililo karibu na mahali ambapo funzo hilo hufanywa.

5 Njia nyingine ya kuwapata watu wengi ni kuhubiri kwenye sehemu za umma. Dada mmoja huko Japani alitaka kuwa painia msaidizi ijapokuwa alikuwa ameajiriwa kazi. Mzee fulani alipendekeza ahubiri barabarani karibu na kituo cha gari-moshi kila siku kabla ya kwenda kazini. Ijapokuwa alikuwa mwenye haya mwanzoni na alidhihakiwa na baadhi ya abiria, sasa anawapelekea watu 40 hivi magazeti kwa ukawaida, wakiwemo abiria, wafanyakazi wa kituo, na wenye maduka kwenye eneo hilo. Kila mwezi aliwaachia watu magazeti 235 kwa wastani. Kwa kuzungumzia Maandiko pamoja na watu kwa dakika chache tu kila siku, aliweza kuanzisha mafunzo sita ya Biblia.

6 Fursa za Kutoa Ushahidi: Wahubiri vijana wanaoenda shuleni hupata likizo mara kadhaa kila mwaka. Inafaa kutumia vipindi hivyo kufanya utumishi wa upainia msaidizi. Isitoshe, vijana Wakristo wanaweza kuongeza utumishi kwa kuwahubiria wanafunzi wenzao shuleni. Huenda ukashangaa kuona kwamba wanafunzi wenzako wana maswali mengi kuhusu imani yako. Kwa nini usitoe ushahidi wakati wa mazungumzo darasani au kwa kuandika insha kuhusu imani yako? Baadhi ya wanafunzi wametoa ushahidi kwa kuonyesha video zetu. Wengine wameanzisha mafunzo ya Biblia na wanafunzi wenzao na kuwasaidia kujiweka wakfu na kubatizwa. Hizo ni njia bora za ‘kulisifu jina la Yehova.’—Zab. 148:12, 13.

7 Katika shughuli zako za kila siku, jitahidi kutumia njia mbalimbali kuzungumza na watu juu ya Mungu wetu mwema na ahadi zake za ajabu. Ndugu mmoja ambaye husafiri kwenye magari-moshi yaleyale kila siku huwahubiria abiria wenzake kila inapofaa. Kwa mfano, alipokuwa akingojea gari-moshi kwenye kituo fulani, alimhubiria mwanamume mmoja kijana kwa muda wa dakika tano hivi kila siku. Kwa sababu hiyo, mwanamume huyo kijana na mfanyakazi mwenzake walikubali kujifunza Biblia. Funzo hilo la Biblia lilifanywa kwenye gari-moshi waliposafiri. Baada ya muda fulani, mwanamke mzee aliyekuwa akisikiliza mazungumzo yao alimwendea ndugu huyo na kuomba funzo la Biblia. Sasa yeye pia hujifunza Biblia kila anaposafiri pamoja na ndugu huyo kwenye gari-moshi. Ndugu huyo amejifunza na watu kumi kwenye magari-moshi.

8 Vipi kama huwezi kufanya mengi kwa sababu ya uzee au matatizo ya afya? Labda unaweza kumsifu Yehova kwa kadiri kubwa zaidi licha ya hali hizo. Je, umewahi kutoa ushahidi kwa kutumia simu? Ikiwa hujui jinsi ya kutoa ushahidi kwa kutumia simu, mweleze mwangalizi wa funzo lenu la kitabu tatizo lako. Huenda akapanga ili wahubiri ambao wamezoea utumishi huo wakusaidie. Mnapohubiri pamoja kwa kutumia simu mnaweza kufunzana na kusaidiana kutoa ushahidi kwa njia bora. Kuna mapendekezo mazuri ya jinsi ya kutumia simu ili kutoa ushahidi katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2001, ukurasa wa 5-6.

9 Huenda wapya wakachochewa kumsifu Yehova zaidi kwa kuhudhuria Ukumbusho. Unaweza kuwasaidia kushinda woga wowote ambao huenda ukawazuia wasijitolee kuwa wahubiri wasiobatizwa kwa kusimulia mambo yenye kutia moyo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani, na kuwazoeza hatua kwa hatua kueleza mafundisho ya Biblia na kutetea imani yao. (1 Pet. 3:15) Mwanafunzi wa Biblia akitaja kwamba anataka kuanza kuhubiri habari njema, ongea na mwangalizi-msimamizi. Yeye atapanga kukutana na mwanafunzi huyo ili aone ikiwa atastahili kuhubiri pamoja na kutaniko. Bila shaka, moyo wa Yehova unashangilia anapowaona wapya wakiunga mkono upande wake katika suala la enzi kuu ya ulimwengu!—Met. 27:11.

10 Je, Unaweza Kuwa Painia Msaidizi? Takwa la saa 50 kwa painia msaidizi linapaswa kuchukuliwa kwa uzito. (Mt. 5:37) Jambo hilo linamaanisha kwamba unahitaji kupanga kutumia kwa wastani muda wa saa 12 kila juma katika utumishi wa shambani. Je, kuna pendekezo linalokufaa katika ratiba za utumishi wa upainia msaidizi kwenye ukurasa wa 5? Ikiwa hakuna, je, unaweza kupanga ratiba yako mwenyewe inayokuwezesha kuwa painia msaidizi mwezi wa Machi, Aprili, au Mei? Mwombe Yehova abariki jitihada zako za kuongeza utumishi.—Met. 16:3.

11 Wazee na watumishi wa huduma watakuunga mkono kabisa unapojitahidi kufanya majira haya ya Ukumbusho yamletee Yehova sifa ya kipekee. Yamkini wengi wao watatumikia kama mapainia wasaidizi. Wazee watapanga mikutano ya ziada ya utumishi, kama vile saa za alasiri, saa za jioni siku za katikati ya juma, na Jumamosi na Jumapili, kulingana na uhitaji. Ili kuamua mahali panapofaa na saa zinazofaa za mikutano hiyo, na pia kuwateua wale watakaoiongoza, wazee wanaweza kuongea na wale ambao wamepanga kuwa mapainia wasaidizi au wale wanaofikiria kufanya utumishi huo. Wazee watajitahidi kupanga mambo ili kuwe na wahubiri unaoweza kuandamana nao katika siku na saa ambazo umetenga kwa ajili ya huduma. Kwa njia hiyo mipango inaweza kufanywa imara na mambo mengi mazuri yanaweza kutimizwa.—Met. 20:18.

12 Fanya Yote Uwezayo: Ikiwa huwezi kuwa painia msaidizi kwa sababu ya hali, kumbuka kwamba Yehova anakubali jitihada na dhabibu zetu “kulingana na kile ambacho mtu anacho, si kulingana na kile ambacho mtu hana.” (2 Kor. 8:12) Tuna sababu nyingi sana za kumshukuru Yehova. Daudi alikuwa na sababu nzuri ya kuandika maneno haya: “Nitambariki Yehova nyakati zote; daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.” (Zab. 34:1) Tuazimie kufanya vivyo hivyo katika majira haya ya Ukumbusho.

[Maswali ya Funzo]

1. Waisraeli waliomwogopa Mungu walifaidikaje na “sherehe za majira”?

2, 3. Kwa nini inafaa kuongeza utumishi wakati wa majira ya Ukumbusho, na tutaadhimisha Ukumbusho siku gani?

4, 5. (a) Baadhi ya wahubiri wamefanya nini ili wawahubirie watu wengi zaidi habari njema? (b) Ni njia gani ambayo ni yenye mafanikio katika eneo lenu?

6. Vijana wanawezaje kuongeza utumishi wao?

7. (a) Ndugu mmoja alitumia fursa gani za kuwahubiria wengine? (b) Je, umewahi kuwahubiria abiria wenzako?

8. Wazee na wale walio na matatizo ya afya wanaweza kuongeza utumishi kwa njia gani?

9. Unawezaje kuwasaidia wanafunzi wa Biblia ili wastahili kuhubiri pamoja na kutaniko?

10. (a) Ratiba nzuri inawezaje kutusaidia kufanya utumishi wa painia msaidizi? (b) Je, ulifaulu kuwa painia msaidizi mwaka uliopita katika majira ya Ukumbusho? Ulifaulu kwa kufanya nini?

11. Wazee na watumishi wa huduma wanawezaje kuwaunga mkono wale watakaotumikia kama mapainia wasaidizi?

12. Ni nini ambacho hutusukuma kumsifu Yehova sikuzote?

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Unawezaje Kuongeza Utumishi Wako?

◼ Kuhubiri wakati ambapo watu wako nyumbani

◼ Kuhubiri kwenye sehemu za umma

◼ Kuhubiri kazini au shuleni

◼ Kutoa ushahidi kwa kutumia simu

◼ Kuwa painia msaidizi

[Chati katika ukurasa wa 5]

Mapendekezo ya Ratiba za Utumishi wa Painia Msaidizi—Njia za Kuhubiri kwa Muda wa Saa 12 Kila Juma

Asubuhi ya Jumatatu Hadi Jumamosi

Unaweza kuhubiri Jumapili badala ya siku moja kati ya zile zilizotajwa.

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Asubuhi 2

Jumanne Asubuhi 2

Jumatano Asubuhi 2

Alhamisi Asubuhi 2

Ijumaa Asubuhi 2

Jumamosi Asubuhi 2

Jumla ya Saa: 12

Siku Mbili

Chagua siku zozote mbili. (Ikitegemea siku ambazo umechagua, ukifuata ratiba hii, huenda ukahitaji kuhubiri muda wa saa mbili zaidi ili kutimiza kiwango cha saa 50 kwa mwezi.)

Siku Kipindi Saa

Jumatano Siku Nzima 6

Jumamosi Siku Nzima 6

Jumla ya Saa: 12

Jioni Mbili, Jumamosi, na Jumapili

Chagua jioni mbili katikati ya juma.

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Jioni 1 1⁄2

Jumatano Jioni 1 1⁄2

Jumamosi Siku Nzima 6

Jumapili Nusu Siku 3

Jumla ya Saa: 12

Alasiri Tatu na Jumamosi

Unaweza kuhubiri Jumapili badala ya siku moja kati zile zilizotajwa.

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Alasiri 2

Jumatano Alasiri 2

Ijumaa Alasiri 2

Jumamosi Siku Nzima 6

Jumla ya Saa: 12

Ratiba Yangu ya Utumishi

Amua utahubiri kwa muda wa saa ngapi kila kipindi.

Siku Kipindi Saa

Jumatatu

Jumanne

Jumatano

Alhamisi

Ijumaa

Jumamosi

Jumapili

Jumla ya Saa: 12

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki