Matangazo
◼ Machi: Tutatoa broshua Endeleeni Kukesha. Mwenye nyumba akipendezwa mtolee kitabu Ujuzi na ujaribu kuanzisha funzo la Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, watembelee pia wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mkutano mwingine lakini ambao hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida na ujitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Lengo lako lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia, hasa na wale ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Tutatoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu lakini mwenye nyumba akisema hana watoto mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Wahubiri wanapaswa kupewa matoleo mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yafikapo. Hilo litawawezesha kufahamu habari iliyomo kabla ya kuyatoa magazeti hayo katika utumishi wa shambani. Pia, wahubiri wanapaswa kupewa Huduma Yetu ya Ufalme mara tu inapofika. Wanaweza kupewa nakala zao kupitia mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa Alhamisi, Machi 24, 2005. Ikiwa kutaniko lenu linafanya mikutano Alhamisi, mikutano hiyo inapaswa kufanywa siku tofauti. Jambo hilo lisipowezekana kwa sababu makutaniko mengine yanatumia Jumba la Ufalme siku zile nyingine, sehemu za Mkutano wa Utumishi zilizo muhimu sana kwa kutaniko lenu zinaweza kushughulikiwa katika Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Wahubiri kadhaa wameuliza kuhusu nyimbo za Ufalme ambazo zimeimbwa kwa mtindo unaopendwa na watu wengi. Nyimbo hizo zimerekodiwa na kuenezwa miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Wahubiri hao wanataka kujua ikiwa nyimbo hizo zina kibali cha tengenezo. Tunafahamu kwamba nyimbo hizo zinaenezwa, nasi tungependa kuwajulisha kuwa hazina kibali chetu. Tafadhali msieneze nyimbo hizo katika Intaneti wala kuzirekodi kutoka kwenye Intaneti. Tunatumaini kwamba jambo hilo limeeleweka vizuri.
◼ Iwapo unapanga kutembelea nchi nyingine, na unataka kujua tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko au kusanyiko, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Unaweza kupata orodha ya anwani za ofisi za tawi katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Fomu hizo zinaweza kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni akiba ya angalau mwaka mzima.