Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Mei 9
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Aprili 15 na Amkeni! la Aprili 22. Mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutumiwa. Katika onyesho moja mhubiri anamtolea abiria mwenzake magazeti wanaposafiri.
Dak. 15: Tumia Neno la Mungu ili Kuufikia Moyo. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 2005, ukurasa wa 28-31. Zungumzia jinsi Yesu alivyotumia Maandiko kumsaidia Petro, na jinsi tunavyoweza kuiga mfano wa Yesu tunapohitaji kurekebisha maoni na hisia za watoto wetu, za wanafunzi wetu wa Biblia, na zetu wenyewe.
Dak. 20: “Panga Ratiba Inayofaa ya Familia.” Katika utangulizi usiozidi dakika mbili, onyesha umuhimu wa kuwa na ratiba iliyoandikwa na uzungumzie jinsi ya kujaza ratiba iliyo kwenye ukurasa wa 6. Kisha zungumzia makala “Ratiba ya Familia—Mikutano ya Kutaniko” kwa maswali na majibu. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamefaulu kupanga shughuli zao ili zisiwazuie kuhudhuria mikutano. Mambo mengine yanayohusu ratiba ya familia yatazungumziwa katika majuma yatakayofuata.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Ratiba ya Familia—Utumishi wa Shambani wa Familia.”a Waombe wasikilizaji waeleze jinsi wanavyonufaika kwa kuhubiri pamoja na familia zao kwa ukawaida.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 9.”b Unapozungumzia fungu la 2, kazia jambo moja au mawili katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 2004, ukurasa wa 8. Panga onyesho fupi la funzo la Biblia. Baada ya kumaliza somo la 2 katika broshua Anataka, mhubiri anayeongoza funzo anamuuliza mwanafunzi swali hili: “Ungemwelezaje rafiki yako kuhusu jina la Mungu?” Mwanafunzi anaeleza jinsi ambavyo angetumia Zaburi 83:18, kisha mhubiri anampongeza.
Wimbo 134 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 23
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa michango. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei 8. Mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutumiwa. Katika onyesho moja mhubiri anatoa magazeti barabarani.
Dak. 18: “Siku ya Yehova Iko Karibu.”c Unapotayarisha sehemu hii, chunguza kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli, ukurasa wa 59, fungu la 28.
Dak. 15: “Ratiba ya Familia—Funzo la Familia.”d Panga mapema mtu mmoja au wawili waeleze kuhusu ratiba yao ya funzo la familia na jitihada zao za kuwa na funzo hilo kwa ukawaida.
Wimbo 152 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Mei. Taja vichapo tutakavyotoa mwezi wa Juni. Onyesha jinsi ya kutoa vichapo hivyo kwa kutumia pendekezo moja au mawili (ikiwa yanafaa katika eneo lenu) katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005. Utangulizi mwingine unaofaa eneo lenu unaweza kutumiwa.
Dak. 20: “Ratiba ya Familia—Andiko la Siku.”e Waombe wasikilizaji waeleze jinsi familia zao zinavyonufaishwa kwa kuchunguza andiko la siku pamoja. Wamepanga ratiba gani inayofaa familia zao?
Dak. 15: Simulia au igiza mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani mwezi wa Machi, Aprili, na Mei. Panga mapema mtu mmoja au wawili waeleze kuhusu jitihada zao za kuhubiri katika majira ya Ukumbusho na baraka walizopata.
Wimbo 115 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Sitawisha Upendezi wa Watu Unaowapelekea Magazeti kwa Ukawaida.”f Unapozungumzia fungu la 3, tumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 313-317. Habari hizo zinaweza kutumiwa kutayarisha mazungumzo yanayotegemea andiko moja kuhusu yale ambayo Ufalme wa Mungu utafanya. Panga onyesho la mhubiri anayezungumzia andiko moja pamoja na mtu ambaye anampelekea magazeti kwa ukawaida. Mhubiri anachagua andiko katika gazeti ambalo ametoka tu kumwachia mwenye nyumba. Anapaswa kuzungumzia andiko hilo kifupi na kutoa mfano ili kumsaidia mwenye nyumba kuelewa jinsi linavyoweza kumnufaisha.
Wimbo 107 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
f Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.