Matangazo
◼ Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, watembelee pia wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mkutano mwingine lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida na ujitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Lengo lako lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia, hasa na wale ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu lakini mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya zile zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them. Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kinaweza kutolewa hasa katika maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu ya kutaniko Juni 1, au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti ya benki ya kushughulikia udumishaji au ujenzi wa Jumba la Ufalme, fanyeni mipango ili kukagua akaunti hiyo pia. Ukaguzi huo unapokamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa taarifa hiyo ripoti ya hesabu itakaposomwa.