Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/05 uku. 5
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2005
Huduma ya Ufalme—2005
km 6/05 uku. 5

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 27, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Mei 2 hadi Juni 27, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Kwa nini inafaa sana kutumia mifano kama vile tashbihi na sitiari tunapofundisha? (Mwa. 22:17; Zab. 1:3; Yak. 3:6) [be uku. 240 fu. 2-4, sanduku]

2. Tunaweza kupata wapi mifano inayofundisha mambo muhimu, lakini tunapaswa kujihadhari na nini tunapotumia mifano? [be uku. 242 fu. 1-2]

3. Tunahitaji kukumbuka nini tunapochagua mifano inayofaa? [be uku. 244 fu. 1-2]

4. Kwa nini tutumie vielelezo tunapofundisha, na Yehova ametumiaje vielelezo? [be uku. 247 fu. 1-2, sanduku]

5. Tunaweza kutumia vielelezo katika utumishi wa shambani jinsi gani? [be uku. 248 fu. 1–uku. 249 fu. 2]

HOTUBA NA. 1

6. Neno la Mungu linatoa mwongozo gani kuhusu kuwasomesha watoto? [w03 3/15 uku. 12 fu. 2; uku. 14 fu. 4]

7. Yehova alionyeshaje kwamba alimpenda Daudi alipokuwa kijana, na Daudi alionyeshaje kwamba alimpenda Yehova? [w03 4/15 uku. 29 fu. 3; uku. 30 fu. 3]

8. Kwa nini Yehova alikubali dhabihu ya Abeli, na jambo hilo linatuhakikishia nini? (Mwa. 4:4) [w03 5/1 uku. 28 fu. 4–uku. 29 fu. 1]

9. Ile “nidhamu ya Yehova” ambayo andiko la Methali 3:11 linatuhimiza tusiikatae ni nini? [w03 10/1 uku. 20 fu. 2-4]

10. “Ujitoshelevu” unaotajwa katika 1 Timotheo 6:6-8, unamaanisha nini? [w03 6/1 uku. 9 fu. 1-2; uku. 10 fu. 1]

USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA

11. Upendo kati ya Yonathani na Daudi unafananisha nini? (2 Sam. 1:26) [w89 1/1 uku. 26 fu. 13]

12. Jaribio la kwanza la Daudi la kupeleka sanduku la agano Yerusalemu linatufundisha nini? (2 Sam. 6:2-9)

13. Baada ya Daudi na Bath-sheba kufanya dhambi, kwa nini mwana wao alikufa, ilhali andiko la Kumbukumbu la Torati 24:16 na Ezekieli 18:20 yanasema kwamba mwana hatakufa kwa sababu ya kosa la baba? (2 Sam. 12:14; 22:31)

14. Tunajuaje kwamba Siba alimshtaki Mefiboshethi kwa uwongo? (2 Sam. 16:1-4)

15. Kwa nini Mefiboshethi alikuwa mfano mzuri kwetu katika kisa kinachomhusu Siba? (2 Sam. 19:24-30)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki