Matangazo
◼ Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu lakini mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them. Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kinaweza kutolewa hasa katika maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida. Septemba: Tunaweza kutoa kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, na broshua Endeleeni Kukesha! iliyo na kurasa 32, au kitabu kingine chochote cha zamani ambacho kinapatikana kutanikoni.
◼ Nakala ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova inapaswa kuwekwa katika maktaba ya Jumba la Ufalme. Mnaweza kupata habari zaidi kuhusu maktaba ya Jumba la Ufalme katika ukurasa wa 5 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2003 na Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997.