Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Taarifa: Huduma Yetu ya Ufalme itapanga Mkutano wa Utumishi wa kila juma wakati wa miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya mabadiliko yanayohitajiwa ili kuwaruhusu watu wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Utii wa Kimungu.” Ikifaa, tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia kusanyiko ili kurudia shauri na vikumbusho vinavyofaa hali zenu vilivyo katika nyongeza ya mwezi huu. Mwezi mmoja au miwili baada ya kuhudhuria kusanyiko, tumieni kati ya dakika 15 na 20 za Mkutano wa Utumishi (mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kwenu) kupitia mambo makuu ya programu ya kusanyiko ambayo yamewafaa wahubiri katika huduma ya shambani. Sote tunaweza kujitayarisha kwa ajili ya pitio hilo kwa kuandika mambo hususa ambayo tutatumia katika huduma ya shambani. Sehemu hiyo ya pekee ya Mkutano wa Utumishi itatupa nafasi ya kueleza jinsi tunavyotumia mambo tuliyojifunza katika kusanyiko na jinsi ambavyo yameboresha huduma yetu. Tutaimarishwa tunapowasikiliza wengine wakieleza jinsi ambavyo wamefuata maagizo tuliyopokea kusanyikoni, nasi tutawatia wengine moyo wafuate ushauri na mapendekezo yaliyotolewa katika kusanyiko hilo.
Juma Linaloanza Juni 13
Dak 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 (ikiwa yanafaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na Amkeni! la Mei 22. Mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutumiwa. Katika onyesho moja mhubiri anatoa magazeti anapohubiri isivyo rasmi.
Dak 15: Kuwasaidia Wengine Wawe Wahubiri Ambao Hawajabatizwa. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mzee yakitegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 79-81. Zungumzia utaratibu unaopaswa kufuatwa ili kuamua ikiwa mwanafunzi wa Biblia ametimiza matakwa ya Kimaandiko na kustahili kuwa mhubiri kutanikoni. Juma lijalo tutazungumzia jinsi tunavyoweza kuwazoeza wanafunzi wa Biblia waliostahili kuwa wahubiri ambao hawajabatizwa waanze kuhubiri nyumba kwa nyumba.
Dak 20: “Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia.”a Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyorejelewa kadiri wakati unavyoruhusu.
Wimbo 149 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 20
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika ukurasa wa 4 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 2003. Eleza jinsi wahubiri wanavyoweza kupata vichapo vya lugha za kigeni. Onyesha jinsi habari hii inayoweza kutumiwa kutanikoni mwenu. Maagizo yoyote ya vichapo vya lugha za kigeni yanapaswa kufanywa kupitia kwa mtumishi wa vitabu, hata kama ni kichapo kimoja tu kinachoagizwa. Kwa kufanya hivyo tutapokea vichapo hivyo kwa wakati.
Dak 15: Neno la Mungu Lina Nguvu. (Ebr. 4:12) Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 2003, ukurasa wa 11, fungu la 13-17. Simulia mambo yaliyoonwa yanayoonyesha jinsi Biblia inavyoweza kuwachochea watu kufanya mabadiliko maishani mwao. (w00 1/1 uku. 3-5) Watie wote moyo watumie Biblia vizuri katika huduma ya shambani.
Dak 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 10.”b Tia ndani onyesho la kipindi cha mazoezi. Mwanafunzi anapojizoeza kuhubiri, mwalimu, ambaye anaigiza sehemu ya mwenye nyumba, anatoa kizuia-mazungumzo ambacho hutolewa kwa ukawaida katika eneo lenu, na mwanafunzi anaposhindwa kukikabili, mwalimu anamweleza jambo la kufanya. Zaidi ya hilo, panga mapema mmoja au wawili waeleze jinsi walivyozoezwa walipoanza kuhubiri nyumba kwa nyumba.
Wimbo 208 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 27
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Juni. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 6 (ikiwa yanafaa eneo lenu), kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni 8. Utoaji mwingine unaofaa eneo lenu unaweza kutumiwa. Baada ya onyesho, rudia tena utangulizi ambao mhubiri alitumia kuamsha upendezi wa mwenye nyumba.
Dak 30: “Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa.” Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Taja kusanyiko ambalo kutaniko lenu limegawiwa kuhudhuria. Pitia mafungu yaliyo na namba kama Funzo la Mnara wa Mlinzi linavyofanywa. Msomaji apewe mgawo wa kusoma mafungu. Pitia sanduku lenye kichwa “Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya.”
Wimbo 196 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 4
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: Je, Mna Ratiba ya Familia? Pitia mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2005, kisha uwaombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamejitahidi kufuata mapendekezo hayo na manufaa ambazo wamepata kwa kufanya hivyo.
Dak 20: “Kupata Matokeo Tunapohubiri Sehemu za Umma.”c Onyesha jinsi habari inavyohusu eneo lenu. Wakumbushe wahubiri watumie fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) inapofaa.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2005, uku. 6.
Wimbo 120 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.