Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 4
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2005
Huduma ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 4

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 29, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Julai 4 hadi Agosti 29, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunapoongea na wengine kuhusu tumaini letu, tunawezaje kufanya ‘usawaziko wetu ujulikane kwa watu wote,’ na kwa nini jambo hilo ni muhimu? (Flp. 4:5; Yak. 3:17) [be uku. 251 fu. 1-3, sanduku]

2. Kutambua inapofaa kubadilikana, hutusaidiaje kusikilizana vizuri na wengine? [be uku. 253 fu. 1-2]

3. Kwa nini ni muhimu kutumia maswali vizuri tunapowasaidia wengine kuelewa sababu ya jambo fulani? [be uku. 253 fu. 3-4]

4. Ni mambo gani yanayopaswa kuzingatiwa ili hotuba au mazungumzo yawe yenye kuvutia? [be uku. 255 fu. 1-4, sanduku; uku. 256 fu. 1, sanduku]

5. Tunapaswa kukumbuka nini tukiamua kutumia uthibitisho ambao hautokani na Biblia ili kuonyesha kwamba jambo fulani katika Maandiko ni la kweli? [be uku. 256 fu. 3-5, sanduku]

HOTUBA NA. 1

6. Kuna uthibitisho gani ulio wazi kwamba Yesu aliishi duniani? [w03 6/15 uku. 4-7]

7. ‘Kinywa cha wanyoofu kinawakomboa’ kwa njia gani, na “nyumba ya waadilifu itaendelea” kusimama kwa njia gani? (Met. 12:6, 7) [w03 1/15 uku. 30 fu. 1-3]

8. Kwa kuwa Biblia si orodha ya mambo tunayopaswa na tusiyopaswa kufanya, tunawezaje ‘kufahamu yale yaliyo mapenzi ya Yehova’? (Efe. 5:17) [w03 12/1 uku. 21 fu. 3–uku. 22 fu. 3]

9. Ni kanuni zipi za Biblia zinazoweza kumsaidia mtu kupambana na umaskini na hali ngumu za uchumi? [w03 8/1 uku. 5 fu. 3-6]

10. Mfano wa Yehova wa kutoa kwa hiari unatuchochea kufanya nini? (Mt. 10:8) [w03 8/1 uku. 20-22]

USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA

11. Nguzo mbili zilizoitwa Yakini na Boazi, ambazo zilikuwa mlangoni pa hekalu lililojengwa na Sulemani zilimaanisha nini? (1 Fal. 7:15-22)

12. Je, tendo la Sulemani la kumpa Mfalme Hiramu wa Tiro zawadi ya majiji 20 katika nchi ya Galilaya lilipatana na Sheria ya Musa?(1 Fal. 9:10-13)

13. Kule kutotii kwa “mtu wa Mungu” kunaweza kutufundisha nini? (1 Fal. 13:1-25)

14. Mfalme Asa wa Yuda alionyeshaje ujasiri wake, na mfano wake unatufundisha nini? (1 Fal. 15:11-13)

15. Kisa kinachomhusu Mfalme Ahabu na Nabothi kinaonyeshaje hatari ya kujisikitikia? (1 Fal. 21:1-16)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki