Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 12
  • Juma Linaloanza Septemba 19
  • Juma Linaloanza Septemba 26
  • Juma Linaloanza Oktoba 3
Huduma ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 2

Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Septemba 12

Wimbo 29

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Agosti 15 na Amkeni! la Agosti 22 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Mapendekezo mengine yanayofaa yanaweza kutumiwa. Onyesho moja lishughulikiwe na mzee wa kutaniko na kijana ashughulikie lile lingine. Baada ya kila onyesho kazia mambo mazuri ya onyesho.

Dak. 20: “Tumia Wakati Wako kwa Hekima.”a Waombe wasikilizaji waeleze jinsi wanavyotenga wakati wa kusoma Biblia kila siku. Mtie moyo mtu mmoja-mmoja na watu wa familia watumie nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2005 kupanga ratiba ya utendaji wa kiroho.

Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo.”b Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Sehemu ya 1 na ya 2 ya nyongeza. Habari nyingine zinapatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2004, ukurasa wa 1. Kwa nini ni muhimu kujitayarisha vizuri kila wakati kabla ya kuongoza funzo la Biblia? Matayarisho hayo yanahusisha nini? Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamefuata mapendekezo yaliyotolewa. Malizia kwa kuzungumzia sanduku lililo juu kwenye ukurasa wa kwanza wa nyongeza.

Wimbo 110 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 19

Wimbo 168

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu ya barua kutoka ofisi ya tawi kwenye ukurasa wa kwanza wa toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 20: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Mwangalizi wa utumishi anapitia utendaji wa mwaka wa utumishi uliopita, na anakazia mambo yenye kutia moyo yaliyofanywa katika huduma. Wapongeze ndugu kwa mambo hususa waliyotimiza. Taja jambo moja au mawili yanayohitaji kufanyiwa maendeleo mwaka huu. Taja kazi ya mapainia, na uwapongeze kwa bidii yao. Eleza kuhusu matokeo mazuri ya jitihada za kuwasaidia wasiotenda waanze kuhubiri tena.

Dak. 15: “Endeleeni Kujengana.”c Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamenufaika kwa sababu wengine wanawajali na kuwapenda.

Wimbo 199 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 26

Wimbo 122

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Septemba.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Tangaza Habari Njema kwa Kutoa Magazeti. Toleo la mwezi wa Oktoba ni magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Katika hotuba ya utangulizi, zungumzia mapendekezo yafuatayo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2005, ukurasa wa 8, fungu la 3-6: (1) Toa magazeti yote mawili. (2) Panga ushiriki katika kazi ya magazeti siku moja kila juma. (3) Kila mwezi, uwe na lengo la kuwaachia watu idadi fulani ya magazeti. (4) Tumia kila fursa inayofaa kutoa magazeti. (5) Tumia magazeti ya zamani. Onyesha jinsi kutaniko lenu linavyoweza kufuata mapendekezo hayo. Kisha, panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Septemba 1 na Amkeni! la Septemba 8 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 katika Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi huu (yakifaa eneo lenu). Mapendekezo mengine yanayofaa yanaweza kutumiwa. Pia, kazia makala za ziada ambazo huenda zikawavutia watu katika eneo lenu. Panga kuwe na onyesho la jinsi mojawapo ya makala hizo inavyoweza kukaziwa gazeti linapotolewa. Baada ya kila onyesho, kazia mambo mazuri ya onyesho.

Wimbo 3 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Oktoba 3

Wimbo 54

Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: “Wasaidie Wengine ‘Watii Kutoka Moyoni.’”d Kukiwa na wakati, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yasiyonukuliwa.

Dak. 20: Kuufanya Moyo wa Yehova Ushangilie. (Met. 27:11) Wahoji wahubiri wawili au watatu ambao wamemtumikia Yehova kwa uaminifu kwa muda mrefu. Mwombe kila mmoja wao ataje jambo moja au mawili ambayo yamemsaidia kuendelea kumtii Yehova. Wanaweza kutaja mambo kama vile kujifunza Biblia kwa bidii, kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, kushirikiana na watumishi wengine washikamanifu, kushiriki katika utumishi wa shambani kwa nafsi yote, kusali kutoka moyoni, na kujiepusha na burudani zisizofaa. Walikabili majaribu gani ya utii, nao walishinda majaribu hayo kwa njia gani? Wamepata baraka gani kwa kuwa watiifu?

Wimbo 170 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki