Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/05 uku. 8
  • Sitawisha Ustadi wa Kujadiliana na Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sitawisha Ustadi wa Kujadiliana na Wengine
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Je! Wewe ni Mwenye Matokeo Katika Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kuwa Wahudumu Wenye Ubunifu, Wanaobadilika Kulingana na Hali
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • “Endelea Kufanya Bidii . . . Katika Kufundisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 10/05 uku. 8

Sitawisha Ustadi wa Kujadiliana na Wengine

1 Hotuba ya Paulo katika sinagogi huko Antiokia ya Pisidia, iliyorekodiwa kwenye Matendo 13:16-41, ni kielelezo kizuri cha jinsi ya kujadiliana na watu wengine. Paulo alifikiria malezi na maoni ya wasikilizaji wake naye alibadili mazungumzo yake kupatana na mambo hayo alipowahubiria habari njema. Tunapochunguza masimulizi hayo, na tufikirie jinsi tunavyoweza kumwiga Paulo katika huduma yetu.

2 Tafuta Mambo Yanayokubalika kwa Mwenye Nyumba: Ingawa ujumbe wa Paulo ulikazia daraka kubwa la Yesu katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu, Paulo hakuanza hotuba yake kwa kutaja jambo hilo. Badala yake, alizungumzia historia ya Wayahudi, jambo ambalo wengi wa wasikilizaji wake ambao walikuwa Wayahudi walikubali. (Mdo. 13:16-22) Vivyo hivyo, tutafanikiwa zaidi kuifikia mioyo ya watu tukitafuta mambo ambayo yanakubalika kwao. Huenda tukahitaji kutumia maswali kwa njia ya busara ili kuwachochea waeleze maoni yao, kisha kuwasikiliza kwa makini ili tutambue mambo yaliyo muhimu kwao.

3 Alipozungumzia historia ya Wayahudi, Paulo aliwakumbusha wasikilizaji wake kuhusu ahadi ya Mungu ya kutokeza Mkombozi katika ukoo wa Daudi. Hata hivyo, Wayahudi wengi walikuwa wakingoja mtu hodari kijeshi ambaye angewakomboa kutoka katika utawala wa Waroma na kulifanya taifa lao kuwa bora kuliko mengine yote. Bila shaka walijua kwamba Yesu alikuwa amekataliwa na viongozi wa dini ya Wayahudi huko Yerusalemu, akatiwa mikononi mwa wakuu wa Roma, na kuuawa. Paulo angewezaje kuwathibitishia kwamba Huyo ndiye Masihi aliyeahidiwa?

4 Badili Njia Yako ya Kujadiliana na Watu: Kwa kuwa Paulo alijua maoni ya wasikilizaji wake, alitumia Maandiko kujadiliana nao juu ya mambo ambayo tayari walikuwa wameyakubali. Kwa mfano, alitaja kwamba Yesu alikuwa mzao wa Daudi na kwamba yeye ndiye aliyetambulishwa na Yohana Mbatizaji ambaye alionwa na wengi kuwa nabii wa Mungu. (Mdo. 13:23-25) Paulo alisema kwamba kwa kumkataa Yesu na kumhukumu kifo, viongozi wa dini “walitimiza mambo yaliyosemwa na Manabii.” (Mdo. 13:26-28) Isitoshe, alieleza kuwahusu watu ambao walishuhudia kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa. Alikazia Maandiko fulani ambayo Wayahudi waliyajua na ambayo yalikuwa yametimizwa katika ufufuo wa Yesu.—Mdo. 13:29-37.

5 Kwa upande mwingine, Paulo alitumia njia tofauti ya kujadili mambo alipozungumza na Wagiriki huko Areopago, jijini Athene. (Mdo. 17:22-31) Hata hivyo, alizungumzia ujumbe uleule, na katika visa vyote viwili alipata matokeo mazuri. (Mdo. 13:42, 43; 17:34) Vivyo hivyo leo, tutapata matokeo mazuri zaidi katika huduma tukitafuta mambo ambayo yanakubalika kwa wasikilizaji wetu, na tukibadili njia yetu ya kujadili mambo ili ipatane na malezi na maoni yao.

[Maswali ya Funzo]

1. Tutachunguza masimulizi gani ya Biblia, na kwa nini?

2. Tunajifunza nini kutokana na njia ambayo Paulo alianza hotuba yake?

3. Ni nini kilichofanya iwe vigumu kwa wasikilizaji wa Paulo kukubali kwamba Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa?

4. Paulo alijadilianaje kwa ustadi na wasikilizaji wake Wayahudi?

5. (a) Paulo alibadilije njia yake ya kujadili mambo alipozungumza na Wagiriki? (b) Tunawezaje kuiga kielelezo cha Paulo tunapohubiri katika eneo letu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki