Pitio la Shule ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 31, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Septemba 5 hadi Oktoba 31, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kuhakikishaje kwamba tunawagusa watu mioyo tunapowafundisha Neno la Mungu? (Mat. 13:19) [be uku. 258 fu. 1-2, na sanduku]
2. Ni nini kinachoweza kutusaidia kumfanya mtu aeleze mambo yaliyo moyoni mwake, lakini tunapaswa kufikiria nini? [be uku. 259 fu. 1-2]
3. Tunapofundisha, kwa nini ni muhimu kukazia sifa bora za Yehova? [be uku. 260 fu. 1]
4. Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi wetu wa Biblia watambue marekebisho wanayopaswa kufanya? [be uku. 260 fu. 4–5]
5. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia au wasikilizaji wetu wachunguze nia yao ya kufanya mambo? [be uku. 262 fu. 1-2]
HOTUBA NA. 1
6. Inamaanisha nini ‘kumtafuta Yehova kwa bidii,’ na tunaweza kuonyeshaje kwamba tunafanya hivyo? (Ebr. 11:6) [w03 8/15 uku. 25 fu. 2; uku. 26 fu. 1-2; uku. 27 fu. 2]
7. Ni nini “kielelezo cha maneno yenye afya,” na wazee wanaweza kuonyeshaje kwamba wanashika kielelezo hicho? (2 Tim. 1:13, 14) [w03 1/1 uku. 29 fu. 3–uku. 30 fu. 1]
8. Ni nini kinachomaanishwa na usemi, “canon ya Biblia,” na ni yapi baadhi ya mambo yanayotumiwa kuamua ikiwa kitabu fulani ni sehemu ya canon ya Biblia? [si uku. 299 fu. 5-6]
9. Kwa nini Kipande cha Muratori, ambacho ni cha sehemu ya mwisho-mwisho ya karne ya pili W.K., ni muhimu sana katika kuthibitisha kwamba Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni sehemu halali ya canon ya Biblia? [si uku. 302 fu. 19]
10. Maandiko yanatoaje haki ya kutafsiri Biblia, nao watafsiri wa kale wa Biblia walitimiza jambo gani muhimu? [si uku. 307 fu. 9]
USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA
11. Je, andiko la 2 Wafalme 13:21 linaunga mkono fundisho la kuabudu mabaki ya vitu vya kale vya kidini?
12. Je, Hezekia alikuwa amefanya mapatano na Misri? (2 Fal. 18:19-21, 25)
13. Ijapokuwa maandishi ya matukio ya kila mwaka ya Waashuri hayaelezi waziwazi ushindi mkubwa wa Yehova juu ya Senakeribu, ni nini kinachokupendeza katika maandishi hayo ya historia? (2 Fal. 19:35, 36)
14. Ni nani aliyekuwa baba ya Shealtieli? (1 Nya. 3:16-18)
15. Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase waliwawekeaje mfano mzuri wote wanaomtumikia Yehova leo? (1 Nya. 5:18-22)