Matangazo
◼ Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatatolewa mwezi wote. Tafadhali wape watu wanaopendezwa broshua Anataka, na uwarudie ukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye-nyumba akisema kwamba hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi au trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Unaweza kutoa vitabu vingine kama vile kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani iwapo vinapatikana kutanikoni. Januari 2006: Tutatoa kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayobadilika rangi au kuwa manjano, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991. Makutaniko yasiyo na vitabu hivyo vya zamani akibani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ikiwa kinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Oktoba una Jumapili tano na Jumamosi tano inafaa sana kufanya utumishi wa upainia msaidizi mwezi huo.
◼ Nyongeza ya toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme ni “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2006” nayo inapaswa kuwekwa ili itumiwe mwaka wa 2006.