Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2006
Maagizo
Katika mwaka wa 2006, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kwa kutegemea utaratibu ufuatao.
VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Toleo la 1992) [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Toleo la 2004) [rs].
Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI kwa wimbo, sala, na utangulizi wa kuwakaribisha wasikilizaji. Kisha fuateni utaratibu ufuatao. Baada ya kila hotuba mwangalizi wa shule atamkaribisha msemaji anayefuata.
SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri-msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, watumishi wa huduma wanaostahili wanaweza kutumiwa.)
HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma anayestahili, nayo itategemea Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hotuba hii ya maagizo itolewe kwa dakika kumi bila maswali ya kurudia. Lengo la kutoa hotuba hii si kuzungumzia tu habari, bali ni kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani, na kukazia mambo ambayo yatanufaisha kutaniko. Kichwa kilichoonyeshwa ndicho kinachopaswa kutumiwa. Ndugu wanaopewa hotuba hii wanapaswa kuzingatia wakati ulioonyeshwa. Ndugu anaweza kushauriwa faraghani inapohitajika.
MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee, au mtumishi wa huduma, anayestahili, atumie dakika tano za kwanza kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu hali zenu. Anaweza kuzungumzia sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Hapaswi kutoa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye manufaa na jinsi inavyowanufaisha. Msemaji anapaswa kuwa mwangalifu asipite zile dakika zake tano za kwanza. Anapaswa kuwaachia wasikilizaji dakika tano ili watoe maelezo yao. Wasikilizaji wanapaswa kuombwa watoe maelezo mafupi (yasiyozidi nusu dakika) kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia na manufaa yake. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu waondoke.
HOTUBA NA. 2: Isizidi dakika 4. Hotuba hii inapaswa kutolewa na akina ndugu. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari hiyo bila kutoa utangulizi wala umalizio. Anapaswa kusoma maandishi ya utangulizi ikiwa amegawiwa kusoma Zaburi. Mwangalizi wa shule atajitahidi hasa kuwasaidia wanafunzi wasome kwa njia inayoeleweka, wawe na ufasaha, wakazie maana kwa njia inayofaa, wawe na ubadilifu wa sauti, watue kwa njia inayofaa, na wasome kwa njia ya maongezi ya kawaida.
HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Hotuba hii inapaswa kutolewa na akina dada. Wanafunzi wanaopewa mgawo huu watapewa au watajichagulia kikao katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani kwenye eneo lenu. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Wanafunzi wapya wapewe hotuba zilizo na marejeo. Mwangalizi wa shule ataangalia hasa jinsi mwanafunzi anavyoeleza habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na mambo makuu. Mwangalizi wa shule atampa msaidizi mmoja.
HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kuzungumzia kichwa kilichoonyeshwa. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Ndugu anapopewa hotuba hii, ataitoa kama hotuba kwa wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa hotuba hii, ataitoa jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Mwangalizi wa shule anaweza kumpa ndugu Hotuba Na. 4 anapoona inafaa kufanya hivyo. Hakikisha kwamba akina ndugu tu ndio wanaopewa hotuba zenye vichwa vilivyo na alama ya nyota.
WAKATI: Hotuba wala maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupita wakati. Wanafunzi wanaotoa Hotuba Na. 2 hadi 4, wanapaswa kukatizwa kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia wakipita wakati, wanapaswa kushauriwa faraghani. Wote wanapaswa kufuata wakati. Programu nzima: Dakika 45, bila kutia ndani wimbo na sala.
SHAURI: Dakika 1. Baada ya kila Hotuba Na. 2, Na. 3, na Na. 4, mwangalizi wa shule atatumia muda usiozidi dakika moja kutoa maelezo yanayojenga kuhusu jambo linalostahili kusifiwa katika hotuba hiyo. Lengo lake si kupongeza tu, bali ni kuonyesha ni kwa nini jambo fulani katika hotuba lilikuwa zuri. Kulingana na uhitaji, baada ya mkutano au katika pindi tofauti, mwanafunzi anaweza kupewa faraghani mashauri yatakayomsaidia afanye maendeleo.
MSHAURI MSAIDIZI: Mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kuchagua mzee mwenye uwezo, ikiwa yupo, awe mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee kadhaa kutanikoni, kila mwaka, mzee tofauti anayestahili anaweza kupewa mgawo huo. Mshauri msaidizi ana daraka la kuwashauri faraghani akina ndugu wanaotoa Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, inapohitajiwa. Hahitaji kuwashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo.
FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu cha shule.
PITIO LA MASWALI NA MAJIBU: Dakika 30. Baada ya kila miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio la maswali na majibu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama inavyoonyeshwa juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio. Ikiwa kutaniko lenu lina kusanyiko la mzunguko katika juma la pitio, mtafanya pitio (na pia sehemu zile nyingine za juma hilo) juma litakalofuata, nazo sehemu zilizo katika ratiba ya juma hilo linalofuata zitatolewa katika kusanyiko hilo la mzunguko. Ikiwa mwangalizi wa mzunguko anatembelea kutaniko lenu katika juma la pitio, wimbo, sifa ya usemi, na mambo makuu ya usomaji wa Biblia zinapaswa kutolewa kama ilivyoonyeshwa katika ratiba. Hotuba ya maagizo (ambayo itatolewa baada ya sifa ya usemi) inapaswa kuwa ile ya juma litakalofuata. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya juma litakalofuata itaanza na sifa ya usemi kisha mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama ilivyoonyeshwa katika ratiba, na hatimaye pitio la maswali na majibu.
RATIBA
Jan. 2 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 29-32 Wimbo 91
Sifa ya Usemi: Faidika Kabisa na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (be uku. 5 ¶1–uku. 8 ¶1)
Na. 1: Furahia Neno la Mungu (be uku. 9 ¶1-5)
Na. 2: 2 Mambo ya Nyakati 30:1-12
Na. 3: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Huepuka Matusi?
Na. 4: Jinsi Dhambi Inavyoathiri Uhusiano Wetu na Mungu (rs uku. 57 ¶2–uku. 58 ¶2)
Jan. 9 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 33-36 Wimbo 144
Sifa ya Usemi: Kusoma kwa Usahihi (be uku. 83 ¶1-5)
Na. 1: 2 Mambo ya Nyakati—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 84 ¶34-36)
Na. 2: 2 Mambo ya Nyakati 34:1-11
Na. 3: Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Nafsi? (rs uku. 222 ¶1–5)
Na. 4: Usione Aibu Kushikamana na Viwango vya Maadili vya Biblia
Jan. 16 Usomaji wa Biblia: Ezra 1-5 Wimbo 137
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusoma kwa Usahihi (be uku. 84 ¶1–uku. 85 ¶3)
Na. 1: Utangulizi wa Ezra (si uku. 85 ¶1-7)
Na. 2: Ezra 1:1-11
Na. 3: Manufaa ya Kuwa na Dhamiri Nyoofu
Na. 4: Wanyama Ni Nafsi (rs uku. 222 ¶6–uku. 223 ¶5)
Jan. 23 Usomaji wa Biblia: Ezra 6-10 Wimbo 106
Sifa ya Usemi: Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 86 ¶1-6)
Na. 1: Ezra—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 87 ¶14-18)
Na. 2: Ezra 6:1-12
Na. 3: Nafsi na Roho Haziendelei Kuishi Baada ya Mtu Kufa (rs uku. 223 ¶6–uku. 226 ¶1)
Na. 4: aMaoni ya Mungu Kuhusu Ndoa
Jan. 30 Usomaji wa Biblia: Nehemia 1-4 Wimbo 161
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 87 ¶1–uku. 88 ¶3)
Na. 1: Utangulizi wa Nehemia (si uku. 88 ¶1-5)
Na. 2: Nehemia 2:1-10
Na. 3: Usalama Ulio Muhimu Zaidi
Na. 4: Roho Takatifu Ni Nini? (rs uku. 242 ¶3–uku. 243 ¶1)
Feb. 6 Usomaji wa Biblia: Nehemia 5-8 Wimbo 40
Sifa ya Usemi: Matamshi Mazuri— Mambo ya Kufikiria (be uku. 89 ¶1–uku. 90 ¶2)
Na. 1: Soma Biblia Kila Siku (be uku. 10 ¶1–uku. 12 ¶3)
Na. 2: Nehemia 5:1-13
Na. 3: Mambo Yanayoonyesha Kwamba Mtu Ana Roho Takatifu (rs uku. 243 ¶3–uku. 244 ¶2)
Na. 4: “Linda Moyo Wako” (Met. 4:23)
Feb. 13 Usomaji wa Biblia: Nehemia 9-11 Wimbo 159
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Matamshi (be uku. 90 ¶3–uku. 91 ¶5)
Na. 1: Kujifunza Amani Badala ya Vita (w04 1/1 uku. 6 ¶8–uku. 7 ¶5)
Na. 2: Nehemia 10:28-37
Na. 3: Mambo Yanayothibitisha Kwamba Yehova Anatupenda
Na. 4: Mwanadamu Hana Roho Inayoendelea Kuishi Baada ya Mwili Kufa (rs uku. 244 ¶6–uku. 245 ¶3)
Feb. 20 Usomaji wa Biblia: Nehemia 12-13 Wimbo 118
Sifa ya Usemi: Ufasaha (be uku. 93 ¶1–uku. 94 ¶3)
Na. 1: Nehemia—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 90-91 ¶16-19)
Na. 2: Nehemia 13:1-14
Na. 3: Kwa Nini Haiwezekani Kuwasiliana na Wafu (rs uku. 140 ¶2–uku. 141 ¶1)
Na. 4: bMichezo ya Jeuri ya Video Haiwafai Wakristo
Feb. 27 Usomaji wa Biblia: Esta 1-5 Wimbo 215
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Ufasaha (be uku. 94 ¶4–uku. 96 ¶3, bila kuzungumzia sanduku kwenye uku. 95)
Pitio la Maswali na Majibu
Mac. 6 Usomaji wa Biblia: Esta 6-10 Wimbo 74
Sifa ya Usemi: Kukabiliana na Kigugumizi (be uku. 95, sanduku)
Na. 1: Utangulizi wa Esta na kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 91-94 ¶1-6, 16-18)
Na. 2: Esta 6:1-10
Na. 3: Jibu la Upole Hugeuza Ghadhabu
Na. 4: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Huepuka Kuwasiliana na Pepo kwa Njia Yoyote Ile? (rs uku. 141 ¶1–uku. 142 ¶6)
Mac. 13 Usomaji wa Biblia: Ayubu 1-5 Wimbo 160
Sifa ya Usemi: Kutua kwa Kufuata Alama za Vituo na Ili Kubadili Mawazo (be uku. 97 ¶1–uku. 98 ¶5)
Na. 1: Utangulizi wa Ayubu (si uku. 95-96 ¶1-6)
Na. 2: Ayubu 2:1-13
Na. 3: Usivutiwe na Nguvu za Mashetani (rs uku. 143 ¶1–uku. 144 ¶1)
Na. 4: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Huepuka Kunung’unika?
Mac. 20 Usomaji wa Biblia: Ayubu 6-10 Wimbo 214
Sifa ya Usemi: Kutua Ili Kutia Mkazo, Kutua Ili Kuruhusu Wasikilizaji Wajibu (be uku. 99 ¶1–uku. 100 ¶4)
Na. 1: Ubora wa Kanuni za Kiroho (w04 10/15 uku. 4 ¶2–uku. 5 ¶3)
Na. 2: Ayubu 7:1-21
Na. 3: Kinachomaanishwa na Kuwa Safi Moyoni
Na. 4: Jinsi Mtu Anavyoweza Kuepuka Uvutano wa Pepo (rs uku. 144 ¶2–uku. 145 ¶1)
Mac. 27 Usomaji wa Biblia: Ayubu 11-15 Wimbo 8
Sifa ya Usemi: Kukazia Maana kwa Njia Inayofaa (be uku. 101 ¶1–uku. 102 ¶3)
Na. 1: “Kazia Uangalifu Jinsi Unavyosikiliza” (be uku. 13 ¶1–uku. 14 ¶5)
Na. 2: Ayubu 12:1-25
Na. 3: Jiepushe na Roho ya Kujitegemea (rs uku. 246 ¶3–247 ¶2)
Na. 4: Kwa Nini Huduma Yetu Huleta Shangwe
Apr. 3 Usomaji wa Biblia: Ayubu 16-20 Wimbo 50
Sifa ya Usemi: Kuboresha Sifa ya Kukazia Maana (be uku. 102 ¶4–uku. 104 ¶4)
Na. 1: Jinsi Tunavyoonyesha Tunampenda Mungu (w04 3/1 uku. 19-21)
Na. 2: Ayubu 16:1-22
Na. 3: Jinsi Yehova Anavyowavuta Watu Wamwabudu
Na. 4: cMadhara ya Kuwa na Kiburi na Kuasi (rs uku. 247 ¶3–248 ¶1)
Apr. 10 Usomaji wa Biblia: Ayubu 21-27 Wimbo 119
Sifa ya Usemi: Kukazia Mawazo Makuu (be uku. 105 ¶1–uku. 106 ¶1)
Na. 1: Kanuni za Kiroho Huthawabisha (w04 10/15 uku. 5 ¶4–uku. 7 ¶2)
Na. 2: Ayubu 24:1-20
Na. 3: Yehova Hutupa Nguvu Ipitayo Ile ya Kawaida
Na. 4: dEpuka Tamaa ya Mwili (rs uku. 248 ¶2)
Apr. 17 Usomaji wa Biblia: Ayubu 28-32 Wimbo 100
Sifa ya Usemi: Kiasi Kinachofaa cha Sauti (be uku. 107 ¶1–uku. 108 ¶5)
Na. 1: Kusikiliza Kwenye Mikutano na Makusanyiko (be uku. 15 ¶1–uku. 16 ¶5)
Na. 2: Ayubu 29:1-25
Na. 3: Usiongozwe na Tamaa ya Macho (rs uku. 248 ¶3–249 ¶1)
Na. 4: Kwa Nini Umati Ulistaajabia Njia ya Yesu ya Kufundisha
Apr. 24 Usomaji wa Biblia: Ayubu 33-37 Wimbo 94
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Kiasi cha Sauti (be uku. 108 ¶6–uku. 110 ¶2)
Pitio la Maswali na Majibu
Mei 1 Usomaji wa Biblia: Ayubu 38-42 Wimbo 154
Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Rekebisha Kiasi cha Sauti (be uku. 111 ¶1–uku. 112 ¶2)
Na. 1: Ayubu—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 100 ¶39-43)
Na. 2: Ayubu 38:1-24
Na. 3: Andiko la Isaya 60:22 Linatimizwaje Leo?
Na. 4: eMatukano na Jeuri Ni Matendo ya Mwili (rs uku. 249 ¶2)
Mei 8 Usomaji wa Biblia: Zaburi 1-10 Wimbo 168
Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Badili Mwendo wa Kuzungumza (be uku. 112 ¶3-6)
Na. 1: Utangulizi wa Zaburi—Sehemu ya 1 (si uku. 101 ¶1-5)
Na. 2: Zaburi 4:1–5:12
Na. 3: Mtumaini Yehova Wala Si Mwanadamu (rs uku. 249 ¶3–4)
Na. 4: Kushika Kielelezo cha Maneno Yenye Afya
Mei 15 Usomaji wa Biblia: Zaburi 11-18 Wimbo 217
Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Kuinua na Kupunguza Sauti (be uku. 113 ¶1–uku. 114 ¶2)
Na. 1: Utangulizi wa Zaburi—Sehemu ya 2 (si uku. 102 ¶6-11)
Na. 2: Zaburi 14:1–16:6
Na. 3: Wakristo Si Sehemu ya Ulimwengu Katika Njia Zipi?
Na. 4: Ni Nani Anayefanya Wanadamu Wateseke? (rs uku. 125 ¶1–2)
Mei 22 Usomaji wa Biblia: Zaburi 19-25 Wimbo 23
Sifa ya Usemi: Zungumza kwa Hisia (be uku. 115 ¶1–uku. 116 ¶4)
Na. 1: Ufahamu Mzuri Huleta Kibali (w04 7/15 uku. 27 ¶4–uku. 28 ¶4)
Na. 2: Zaburi 22:1-22
Na. 3: Kuteseka Kulianzaje? (rs uku. 125 ¶3–uku. -126 ¶1)
Na. 4: fVikumbusho vya Mungu Ni Nini, na kwa Nini Tunapaswa Kuvifuata?
Mei 29 Usomaji wa Biblia: Zaburi 26-33 Wimbo 203
Sifa ya Usemi: Shauku Ifae Habari (be uku. 116 ¶5–uku. 117 ¶4)
Na. 1: Unaweza Kuboresha Kumbukumbu Yako (be uku. 17 ¶1–uku. 19 ¶1)
Na. 2: Zaburi 30:1–31:8
Na. 3: Ukweli Unatuwekaje Huru?
Na. 4: Jinsi Tunavyoweza Kuepuka Kuteseka Sana? (rs uku. 126 ¶2-3)
Juni 5 Usomaji wa Biblia: Zaburi 34-37 Wimbo 167
Sifa ya Usemi: Kuonyesha Huruma (be uku. 118 ¶1–uku. 119 ¶5)
Na. 1: Nguvu ya Sala (w04 8/15 uku. 18 ¶6–uku. 19 ¶10)
Na. 2: Zaburi 34:1-22
Na. 3: Kwa Nini Mungu wa Upendo Ameruhusu Kuteseka Kuendelee Muda Mrefu (rs uku. 127 ¶2)
Na. 4: Tunapaswa Kukimbia Aina Zipi za Ibada ya Sanamu?
Juni 12 Usomaji wa Biblia: Zaburi 38-44 Wimbo 216
Sifa ya Usemi: Kuonyesha Hisia (be uku. 119 ¶6–uku. 120 ¶4)
Na. 1: Jinsi Roho ya Mungu Inavyotusaidia Kukumbuka (be uku. 19 ¶2–uku. 20 ¶3)
Na. 2: Zaburi 40:1-17
Na. 3: Sayansi ya Kweli Haipingani na Biblia
Na. 4: Mungu Atayaondoa Madhara Yote Ambayo Yamewapata Watumishi Wake (rs uku. 127 ¶3–uku. 128 ¶1)
Juni 19 Usomaji wa Biblia: Zaburi 45-51 Wimbo 104
Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Ishara za Mwili na za Uso (be uku. 121 ¶1-4)
Na. 1: Yesu Angekuja Lini? (w04 3/1 uku. 16, sanduku)
Na. 2: Zaburi 46:1–47:9
Na. 3: Kwa Nini Mungu Hakumsamehe Adamu (rs uku. 128 ¶2-3)
Na. 4: Mkristo Anawezaje Kuwa Mwenye Nguvu Anapokuwa Dhaifu? (2 Kor. 12:10)
Juni 26 Usomaji wa Biblia: Zaburi 52-59 Wimbo 103
Sifa ya Usemi: Kutoa Ishara za Mwili na za Uso (be uku. 122 ¶1–uku. 123 ¶2)
Pitio la Maswali na Majibu
Julai 3 Usomaji wa Biblia: Zaburi 60-68 Wimbo 45
Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Shambani (be uku. 124 ¶1–uku. 125 ¶4)
Na. 1: Unyenyekevu wa Yehova Unamaanisha Nini Kwetu? (w04 11/1 uku. 29-30)
Na. 2: Zaburi 60:1–61:8
Na. 3: Je, Kushiriki Katika Utendaji wa Kikristo Kunatupa Kibali cha Kuvunja Sheria za Mungu?
Na. 4: Mungu Hasababishi Kasoro za Mwili na Akili (rs uku. 128 ¶4–uku. 129 ¶1)
Julai 10 Usomaji wa Biblia: Zaburi 69-73 Wimbo 225
Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Unapotoa Hotuba (be uku. 125 ¶5–uku. 127 ¶1)
Na. 1: Jitahidi Uwe Msomaji Mzuri? (be uku. 21 ¶1–uku. 23 ¶3)
Na. 2: Zaburi 71:1-18
Na. 3: Kwa Sababu ya Upendo wa Yehova, Watoto Pia Wanaweza Kufaidika Kutokana na Dhabihu ya Fidia ya Kristo (rs uku. 129 ¶2)
Na. 4: gKwa Nini Wakristo Hawapaswi Kuwa na Ubaguzi
Julai 17 Usomaji wa Biblia: Zaburi 74-78 Wimbo 28
Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Shambani (be uku. 128 ¶1–uku. 129 ¶1)
Na. 1: Soma Ukiwa na Makusudi Mazuri (be uku. 23 ¶4–uku. 26 ¶5)
Na. 2: Zaburi 75:1–76:12
Na. 3: Kumtafuta Yehova Kunamaanisha Nini? (Sef. 2:3)
Na. 4: Mungu Hatumii Misiba ya Asili Kuwaadhibu Wanadamu (rs uku. 129 ¶3–uku. 130 ¶2)
Julai 24 Usomaji wa Biblia: Zaburi 79-86 Wimbo 112
Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Jukwaani (be uku. 129 ¶2–uku. 129 ¶5)
Na. 1: “Hema la Wanyoofu Litasitawi” (w04 11/15 uku. 26 ¶1–uku. 28 ¶2)
Na. 2: Zaburi 82:1–83:18
Na. 3: Kupatwa na Taabu Hakumaanishi Kwamba Mtu Hana Kibali cha Mungu (rs uku. 130 ¶3-4)
Na. 4: Je, Kweli Wanadamu Wasiokamilika Wanaweza Kumpendeza Mungu?
Julai 31 Usomaji wa Biblia: Zaburi 87-91 Wimbo 57
Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Unaposoma Mbele ya Watu (be uku. 130 ¶1-3)
Na. 1: ‘Ujuzi Unapokuwa Jambo Rahisi’ na Hekima Inapotuongoza (w04 11/15 uku. 28 ¶3–uku. 29 ¶7)
Na. 2: Zaburi 89:1-21
Na. 3: Kujifunza Biblia Ni Sehemu ya Ibada Yetu
Na. 4: Ufanisi Haupaswi Kuonwa Kuwa Uthibitisho wa Baraka Kutoka kwa Mungu (rs uku. 130 ¶5–uku. 131 ¶1)
Ago. 7 Usomaji wa Biblia: Zaburi 92-101 Wimbo 190
Sifa ya Usemi: Kuwa Safi Hupamba Ujumbe Wetu (be uku. 131 ¶1-3)
Na. 1: Jinsi ya Kujifunza (be uku. 27 ¶1–uku. 31 ¶2)
Na. 2: Zaburi 92:1–93:5
Na. 3: Je, Kusema kwa Lugha Kunaonyesha Kwamba Mtu Ana Roho ya Mungu? (rs uku. 120 ¶2–uku. 121 ¶1)
Na. 4: Umuhimu wa Utimilifu
Ago. 14 Usomaji wa Biblia: Zaburi 102-105 Wimbo 1
Sifa ya Usemi: Jinsi Sifa ya Kiasi na Utimamu wa Akili Zinavyohusika Katika Kuvaa na Kujipamba Kwetu (be uku. 131 ¶4–uku. 132 ¶3)
Na. 1: “Jinsi Kazi Zako Zilivyo Nyingi, Ee Yehova!” (w04 11/15 uku. 8-9)
Na. 2: Zaburi 104:1-24
Na. 3: Kwa Nini Tuendelee Kulinda?
Na. 4: Kwa Nini Kusema kwa Lugha Leo Kunatofautiana na Kule kwa Wakristo wa Karne ya Kwanza? (rs uku. 121 ¶2–uku. 121 ¶5)
Ago. 21 Usomaji wa Biblia: Zaburi 106-109 Wimbo 201
Sifa ya Usemi: Manufaa ya Kuvaa Mavazi Yenye Mpangilio Mzuri (be uku. 132 ¶4–uku. 133 ¶1)
Na. 1: Vijana—Msiwafuate Marika Wenu Bila Kufikiri (w04 10/15 uku. 22 ¶4–uku. 24 ¶4)
Na. 2: Zaburi 107:20-43
Na. 3: Neno la Mungu Hutusaidia Kusababu Kuhusu Madai ya Watu Kwamba Wana Roho ya Mungu (rs uku. 122 ¶2-5)
Na. 4: Tunaweza Kumwigaje Mungu?
Ago. 28 Usomaji wa Biblia: Zaburi 110-118 Wimbo 125
Sifa ya Usemi: Kwa Kuwa Nadhifu Hatutawakwaza Wengine (be uku. 133 ¶2-4)
Pitio la Maswali na Majibu
Sept. 4 Usomaji wa Biblia: Zaburi 119 Wimbo 59
Sifa ya Usemi: Kusimama Vizuri na Kuwa na Vifaa Nadhifu (be uku. 133 ¶5–uku. 134 ¶4)
Na. 1: Funzo Lina Faida (be uku. 31 ¶3–uku. 32 ¶3)
Na. 2: Zaburi 119:25-48
Na. 3: Kwa Nini Tutii Mamlaka za Serikali?
Na. 4: Kusema kwa Lugha Hakuwatambulishi Wakristo wa Kweli Leo (rs uku. 122 ¶6–uku. 123 ¶1)
Sept. 11 Usomaji wa Biblia: Zaburi 120-134 Wimbo 65
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kupunguza Wasiwasi (be uku. 135 ¶1–uku. 137 ¶2)
Na. 1: Jinsi ya Kufanya Utafiti (be uku. 33 ¶1–uku. 35 ¶2)
Na. 2: Zaburi 121:1–123:4
Na. 3: Zawadi ya Kusema kwa Lugha Ingedumu Hadi Lini? (rs uku. 123 ¶2–3)
Na. 4: Kutilia Chumvi Kunamaanisha Nini, na Yesu Alitumiaje Mbinu Hiyo?
Sept. 18 Usomaji wa Biblia: Zaburi 135-141 Wimbo 97
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuwa Mtulivu (be uku. 137 ¶3–uku. 138 ¶5)
Na. 1: Zaburi—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa—Sehemu ya 1 (si uku. 104-105 ¶23-27)
Na. 2: Zaburi 136:1-26
Na. 3: Ukumbusho Ni Mlo wa Ushirika Katika Njia Gani?
Na. 4: hFundisho la Utatu Halitokani na Biblia (rs uku. 367 ¶4–uku. 374 ¶1)
Sept. 25 Usomaji wa Biblia: Zaburi 142-150 Wimbo 5
Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Kukuza Sauti (be uku. 139 ¶1–uku. 140 ¶1)
Na. 1: Zaburi—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa—Sehemu ya 2 (si uku. 105-106 ¶28-32)
Na. 2: Zaburi 142:1–143:12
Na. 3: iMtu Akikuuliza, ‘Je, Unaamini Utatu?’ (rs uku. 389 ¶1–uku. 390 ¶2)
Na. 4: Tunaweza Kutangulizaje Masilahi ya Wengine Mbele ya Masilahi Yetu Wenyewe?
Okt. 2 Usomaji wa Biblia: Methali 1-6 Wimbo 111
Sifa ya Usemi: Kutumia Kikuza-Sauti Vizuri (be uku. 140 ¶2–uku. 142 ¶1)
Na. 1: Utangulizi wa Methali—Sehemu ya 1 (si uku. 106-107 ¶1-5)
Na. 2: Methali 5:1-23
Na. 3: Kwa Nini Kuna Uovu Mwingi Sana? (rs uku. 351 ¶1-4)
Na. 4: jUsieneze Hadithi za Uwongo (2 Tim. 4:4)
Okt. 9 Usomaji wa Biblia: Methali 7-11 Wimbo 73
Sifa ya Usemi: Kutumia Biblia Kujibu Maswali (be uku. 143 ¶1-3)
Na. 1: Utangulizi wa Methali—Sehemu ya 2 (si uku. 107-108 ¶6-11)
Na. 2: Methali 7:1-27
Na. 3: Kutokuwamo kwa Kikristo Husaidia Kudumisha Umoja Wetu
Na. 4: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu? (rs uku. 352 ¶1–uku. 353 ¶1)
Okt. 16 Usomaji wa Biblia: Methali 12-16 Wimbo 180
Sifa ya Usemi: Kuboresha Uwezo Wetu wa Kutumia Biblia (be uku. 144 ¶1-4)
Na. 1: Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti (be uku. 35 ¶3–uku. 38 ¶4)
Na. 2: Methali 14:1-21
Na. 3: Tumefaidikaje kwa Sababu ya Mungu Kuruhusu Uovu Uendelee? (rs uku. 353 ¶2–uku. 354 ¶1)
Na. 4: Ni Nini Kinachoweza Kutusaidia Kukaza Fikira Mikutanoni?
Okt. 23 Usomaji wa Biblia: Methali 17-21 Wimbo 131
Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia (be uku. 145-146)
Na. 1: Methali—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa—Sehemu ya 1 (si uku. 109-110 ¶19-28)
Na. 2: Methali 17:1-20
Na. 3: Jinsi Wakristo Wanavyowaona Wale Walio Wazee kwa Umri
Na. 4: kBiblia Inafundisha Nini Kuhusu Jinsi Tunavyopaswa Kuwaona Wanawake? (rs uku. 400 ¶2-3)
Okt. 30 Usomaji wa Biblia: Methali 22-26 Wimbo 9
Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko (be uku. 147 ¶1–uku. 148 ¶2)
Pitio la Maswali na Majibu
Nov. 6 Usomaji wa Biblia: Methali 27-31 Wimbo 51
Sifa ya Usemi: Kuchagua Maneno Yanayofaa ya Kutanguliza Andiko (be uku. 148 ¶3–uku. 149 ¶3)
Na. 1: Methali—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa—Sehemu ya 2 (si uku. 110-111 ¶29-38)
Na. 2: Methali 28:1-18
Na. 3: Je, Kuwapa Wanaume Ukichwa Ni Kuwashushia Wanawake Heshima? (rs uku. 401 ¶1-3)
Na. 4: Kwa Nini Hatupaswi Kuwahukumu Watu Tunaowakuta Shambani kwa Kutazama Sura Yao?
Nov. 13 Usomaji wa Biblia: Mhubiri 1-6 Wimbo 25
Sifa ya Usemi: Mkazo Unaofaa Unatia Ndani Hisia (be uku. 150 ¶1-2)
Na. 1: Utangulizi wa Mhubiri (si uku. 112-113 ¶1-8)
Na. 2: Mhubiri 5:1-15
Na. 3: Wenye Hekima na Wenye Akili Wamefichwa Kweli za Biblia kwa Njia Gani? (Mt. 11:25)
Na. 4: Je, Wanawake Wanapaswa Kuwa Wahudumu? (rs uku. 402 ¶1-2)
Nov. 20 Usomaji wa Biblia: Mhubiri 7-12 Wimbo 37
Sifa ya Usemi: Kukazia Maneno Yanayofaa (be uku. 150 ¶3–uku. 151 ¶2)
Na. 1: Mhubiri—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 114 ¶15-19)
Na. 2: Mhubiri 9:1-12
Na. 3: Kwa Nini Wanawake Wakristo Hufunika Kichwa Katika Pindi Fulani? (rs uku. 402 ¶3–uku. 403 ¶1)
Na. 4: Kwa Nini Wivu Ni Mbaya?
Nov. 27 Usomaji wa Biblia: Wimbo wa Sulemani 1-8 Wimbo 11
Sifa ya Usemi: Njia za Kutia Mkazo (be uku. 151 ¶3–uku. 152 ¶5)
Na. 1: Utangulizi wa Wimbo wa Sulemani na kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 115-117 ¶1-4, 16-18)
Na. 2: Wimbo wa Sulemani 7:1–8:4
Na. 3: Kwa Nini Wakristo Wanapaswa Kuwa Nadhifu, Safi, na Kuvalia kwa Kiasi?
Na. 4: Je, Ni Sawa Mwanamke Ajipambe kwa Vipodozi na Vito? (rs uku. 404 ¶1-3)
Des. 4 Usomaji wa Biblia: Isaya 1-5 Wimbo 90
Sifa ya Usemi: Kutumia Maandiko Vizuri (be uku. 153 ¶1–uku. 154 ¶3)
Na. 1: Utangulizi wa Isaya (si uku. 118-119 ¶1-8)
Na. 2: Isaya 3:1-15
Na. 3: Je, Ulimwengu Itaharibiwa kwa Moto? (rs uku. 341 ¶1-2)
Na. 4: lKwa Nini Wakristo Hawapaswi Kuwa ‘Wepesi wa Ghadhabu’ (Yak. 1:19)
Des. 11 Usomaji wa Biblia: Isaya 6-10 Wimbo 204
Sifa ya Usemi: Kuonyesha Vizuri Jinsi Andiko Linavyohusika (be uku. 154 ¶4–uku. 155 ¶4)
Na. 1: Kutayarisha Muhtasari (be uku. 39-42)
Na. 2: Isaya 10:1-14
Na. 3: Kwa Nini Ni Muhimu Sana Kuwa Mwenye Kusamehe?
Na. 4: Ni Nani Anayetawala Ulimwengu Huu —Mungu au Shetani? (rs uku. 341 ¶3–uku. 342 ¶2)
Des. 18 Usomaji wa Biblia: Isaya 11-16 Wimbo 47
Sifa ya Usemi: Kutumia Maandiko Kutoa Sababu (be uku. 155 ¶5–uku. 156 ¶5)
Na. 1: Vijana—Acheni Wazazi Wenu Wawasaidie Kulinda Mioyo Yenu (w04 10/15 uku. 20 ¶1–uku. 22 ¶3)
Na. 2: Isaya 11:1-12
Na. 3: Wakristo Huuonaje Ulimwengu na Wale Walio Sehemu ya Ulimwengu? (rs uku. 342 ¶3–uku. 343 ¶4)
Na. 4: Wakristo wa Kweli Hawatapigana Katika Vita vya Har-Magedoni
Des. 25 Usomaji wa Biblia: Isaya 17-23 Wimbo 53
Sifa ya Usemi: Kuonyesha Wasikilizaji Jinsi ya Kutumia Habari (be uku. 157 ¶1–5)
Pitio la Maswali na Majibu
[Maelezo ya Chini]
a Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
b Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
c Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
d Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
e Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
f Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
g Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
h Chagua mambo makuu machache katika habari uliyopewa ambayo yanafaa zaidi eneo lenu.
i Chagua mambo makuu machache katika habari uliyopewa ambayo yanafaa zaidi eneo lenu.
j Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
k Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.
l Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.