Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/05 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 14
  • Juma Linaloanza Novemba 21
  • Juma Linaloanza Novemba 28
  • Juma Linaloanza Desemba 5
Huduma ya Ufalme—2005
km 11/05 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Novemba 14

Wimbo 220

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na Amkeni! la Oktoba 22 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Njia nyingine zinazofaa zinaweza kutumiwa. Katika maonyesho yote mawili, wahubiri wanapaswa kushughulikia kizuia-mazungumzo, “Nina dini yangu mwenyewe,” kwa njia mbili tofauti.—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 18-19.

Dak. 15: Michango Inayoufurahisha Moyo wa Mungu. Hotuba hii inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2005, ukurasa wa 26-30, itolewe na mzee. Gazeti hili lisipopatikana, tumieni makala “Je, Unatambua Furaha Inayotokana na Kutoa?” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2004, ukurasa wa 19-23.

Dak. 20: “Tangazeni Utukufu wa Yehova.”a Unapozungumzia fungu la 4, waombe wasikilizaji waeleze kifupi jinsi mwenendo mzuri unavyoweza kutupa fursa ya kutoa ushahidi.

Wimbo 24 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 21

Wimbo 40

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: Mfanye Yehova Awe Mungu Wako. Hotuba hii inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 2005, ukurasa wa 25-28, itolewe na mzee. Onyesha jinsi tunavyoweza kutumia maishani yale tunayojifunza kumhusu Abrahamu, Daudi, na Eliya.

Dak. 15: “Onyesha Unawajali Watu Kikweli kwa Kuwa Mwenye Utambuzi.”b Panga onyesho la mhubiri anayetambua jambo fulani linalompendeza mwenye nyumba na kubadili mazungumzo kulingana na hilo.

Wimbo 67 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 28

Wimbo 7

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Novemba. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba 8 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Njia nyingine zinazofaa zinaweza kutumiwa. Taja mpango wa michango ya hiari.

Dak. 15: “Tunaweza Kusaidiaje?” Hotuba. Taja visa vichache kuhusu jinsi ambavyo watumishi wa Yehova wamejitahidi kuwasaidia waamini wenzao katika hali ya dharura. (Ona toleo la Amkeni! la Agosti 8, 2003, uku. 10-15; Novemba 22, 2002, uku. 19-24; na Oktoba 22, 2001, uku. 23-27. Visa vingine vilivyochapishwa vinaweza kutajwa pia.) Kisha, zungumzia mambo makuu ya makala iliyo kwenye ukurasa wa 7 wa Huduma Yetu ya Ufalme. Kazia kwamba ikiwa mtu yeyote anataka kutoa mchango ili kuwasaidia ndugu wenye uhitaji wa kimwili, inapendekezwa aweke mchango wake katika sanduku la kazi ya ulimwenguni pote.

Dak. 18: Kuhubiri Habari Njema Katika Mwezi wa Desemba. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Katika hotuba ya utangulizi ya dakika tano, pitia kifupi habari zifuatazo katika makala, “Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo,” inayopatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, ukurasa wa 8: (1) Kwa kawaida tutakuwa na matokeo zaidi tukitumia maneno yetu wenyewe. (2) Tunahitaji kuwa na busara na kubadili mazungumzo yetu ili yafae watu katika eneo letu. (3) Tunahitaji kufikiria malezi na maoni ya watu katika eneo letu. (4) Tunapaswa kusoma kwa makini makala au sura tunayotaka kuzungumzia na kutafuta mambo ambayo huenda yakaamsha upendezi. (5) Si lazima tutumie mapendekezo katika makala hiyo. Zungumzia jinsi ya kufuata maagizo hayo kuhusiana na toleo la Desemba. Unaweza kutumia mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Panga kuwe na onyesho moja au mawili.

Wimbo 123 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 5

Wimbo 38

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 20: “Mheshimu Yehova Katika Maisha Yako Sehemu ya 1—Katika Familia.”c

Dak. 20: “Huduma Yetu Inatimiza Nini?”d Unapozungumzia fungu la 5, tia ndani maelezo yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2004, ukurasa wa 32.

Wimbo 26 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki