Matangazo
◼ Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Unaweza kutoa vitabu vingine kama vile kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani iwapo vinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Januari 2006: Kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991 kinaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo vya zamani akibani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ikiwa kinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo hayana kitabu hiki yanaweza kutoa kitabu kingine cha zamani kinachopatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Machi: Toeni kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidini kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 2006 itatumwa hivi karibuni.
◼ Tungependa kuwajulisha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2007 utakuwa Jumatatu, Aprili 2, baada ya jua kutua. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya maagano pamoja na wasimamizi wa jumba watakalokodi ili kuhakikisha kwamba Ukumbusho unaadhimishwa kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo.
◼ Kwa sababu Ukumbusho ni tukio muhimu, baraza la wazee linapaswa kumteua mzee anayestahili zaidi atoe hotuba ya Ukumbusho badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo ambaye ni mtiwa-mafuta, apewe mgawo huo.
◼ Vitabu na magazeti yote yaliyopo yahesabiwe Desemba 31, 2005 au haraka iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu, na jumla ziandikwe kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa watumishi wa magazeti. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu anapaswa kusimamia kazi hiyo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watie sahihi fomu hiyo. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Tafadhali tumeni nakala ya kwanza kwa ofisi ya tawi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa ili kufanyia hesabu.