Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo kwa Kutumia Kitabu Biblia Inafundisha
Wengi wetu tungefurahia kuongoza funzo la Biblia kama tungefaulu kulianzisha. Kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? kinaweza kutusaidia. Utangulizi kwenye ukurasa wa 3-7 umekusudiwa kutumiwa kuanzisha mazungumzo ya Biblia yanayotegemea kitabu hicho. Hata wale wasio na uzoefu katika utumishi wataona kwamba ni rahisi kuanzisha mafunzo kwa kutumia utangulizi huo.
◼ Jaribu kuanzisha funzo kwa kuzungumzia ukurasa wa 3:
Baada ya kutaja habari fulani ya karibuni au tatizo linalowasumbua watu katika eneo lenu, mwonyeshe mwenye nyumba maswali yaliyoandikwa kwa herufi nzito kwenye ukurasa wa 3, na umuulize maoni yake. Kisha zungumzia ukurasa wa 4-5.
◼ Au huenda ukapenda kuanza kwa kuzungumzia ukurasa wa 4-5:
Unaweza kuuliza hivi: “Tungefurahi sana kuona mabadiliko haya, sivyo?” Au unaweza kuuliza: “Ungetaka kuona utimizo wa ahadi gani kati ya hizi?” Msikilize kwa makini anapotoa maoni yake.
Mwenye nyumba akipendezwa na andiko fulani hususa, mwonyeshe kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu habari hiyo kwa kuzungumzia mafungu yanayofafanua andiko hilo katika kitabu. (Ona sanduku kwenye ukurasa huu.) Zungumzia habari hiyo jinsi ambavyo ungeizungumzia unapoongoza funzo la Biblia. Unaweza kutumia dakika tano hadi kumi kuzungumzia habari hiyo mlangoni unapomtembelea mtu mara ya kwanza.
◼ Unaweza pia kutumia ukurasa wa 6 ili kumchochea mtu atoe maoni yake:
Mwonyeshe mwenye nyumba maswali yaliyo kwenye ukurasa wa sita, na umuulize hivi: “Je, umewahi kujiuliza maswali haya?” Akipendezwa na swali fulani, zungumzia mafungu ya kitabu yanayojibu swali hilo. (Ona sanduku kwenye ukurasa huu.) Unapozungumzia habari hiyo pamoja na mwenye nyumba unaongoza funzo la Biblia.
◼ Unaweza kutumia ukurasa wa 7 kumwonyesha mwenye nyumba jinsi ya kujifunza Biblia:
Soma sentensi tatu za kwanza kwenye ukurasa huo, kisha ufungue sura ya 3 na umwonyeshe mwenye nyumba jinsi ya kujifunza kwa kutumia fungu la 1-3. Panga kumrudia ili mzungumzie majibu ya maswali yaliyo katika fungu la 3.
◼ Jinsi ya kupanga ziara ijayo:
Unapomalizia mazungumzo katika ziara ya kwanza, fanya mpango ili mwendelee na mazungumzo. Unaweza kusema: “Kwa dakika chache tu tumeona kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu habari fulani muhimu. Siku nyingine tunaweza kuzungumzia [taja swali mtakalozungumzia]. Unaonaje nikija wakati kama huu juma lijalo?”
Tunapokaribia wakati uliowekwa, Yehova anaendelea kututayarisha kwa kazi inayopaswa kufanywa. (Mt. 28:19, 20; 2 Tim. 3:17) Na tutumie kitabu hicho kipya kizuri ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.
[Sanduku katika ukurasa wa 3]
Mafungu Yanayozungumzia Maandiko Yaliyo Kwenye Ukurasa wa 4-5
◻ Ufunuo 21:4 (uku. 27-28, fu. 1-3)
◻ Isaya 33:24; 35:5, 6 (uku. 36, fu. 22)
◻ Yohana 5:28, 29 (uku. 72-73, fu. 17-19)
◻ Zaburi 72:16 (uku. 34, fu. 19)
Majibu ya Maswali Yaliyo Kwenye Ukurasa wa 6
◻ Kwa nini tunateseka? (uku. 108-109, fu. 6-8)
◻ Tunawezaje kushughulika na mahangaiko ya maisha? (uku. 184-185, fu. 1-3)
◻ Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha zaidi? (uku. 142, fu. 20)
◻ Inakuwaje tunapokufa? (uku. 58-59, fu. 5-6)
◻ Je, tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa? (uku. 72-73, fu. 17-19)
◻ Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu wakati ujao? (uku. 24, fu. 17)