Funua Nguvu za Neno la Mungu Katika Huduma Yako
Ikiwa mtu anakubali kusikiliza habari njema, tunatumia fursa hiyo vizuri kufunua nguvu za Neno la Mungu kwa kusoma maandiko moja kwa moja kutoka kwenye Biblia. Jambo hilo lilikaziwa katika kusanyiko la pekee la mwaka uliopita. Mwangalizi wa mzunguko alitoa hotuba yenye kichwa “Funua Nguvu za Neno la Mungu Katika Huduma Yako.” Je, unakumbuka mambo makuu?
Kwa nini Neno la Yehova ni lenye nguvu zaidi kuliko maneno yetu?—2 Tim. 3:16, 17.
Ni kwa njia gani Biblia inachochea hisia, inarekebisha fikira, nia na tabia?—Ona Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 2012, uku. 27, fu. 7.
Tunaposoma andiko na mtu fulani katika utumishi, tunawezaje kuzungumzia Biblia kwa njia ambayo inaonyesha kwamba tunaiheshimu?—Ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 148, fu. 3-4 na Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2013, uku. 6, fu. 8.
Kwa nini ni muhimu kueleza na kufafanua maandiko tuliyosoma, nasi tunawezaje kufanya hivyo?—Mdo. 17:2, 3; ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 154, fu. 4 hadi uku. 156, fu. 5.