Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 4
JUMA LINALOANZA MEI 4
Wimbo 68 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 24 ¶1-10 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 1-3 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Samweli 2:24-32 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Uhai wa Kibinadamu wa Yesu Ulilipwa Kuwa “Fidia kwa Ajili ya Wote”—td 6A (Dak. 5)
Na. 3: Ahadi za Biblia Zitakazotimizwa Hivi Karibuni—igw uku. 16 ¶4-uku. 17 ¶1 (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Tembeeni kama watu wenye hekima kwa ‘kujinunulia wakati unaofaa.’—Efe. 5:15, 16.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko. Yanaweza kutia ndani onyesho la jinsi ya kutoa magazeti.
Dak. 5: Machapisho Yatakayotolewa Mwezi wa Mei na Juni. Mazungumzo. Zungumzia jinsi ya kutoa machapisho hayo. Panga kuwe na onyesho.
Dak. 15: Kuhubiri Katika Eneo la Mbali ni Njia Nzuri ya Kutumia Wakati! Mazungumzo. Sehemu hii ishughulikiwe na mzee, ambaye amewahi kuhubiri katika eneo la mbali. Onyesha video Kuhubiri Katika Eneo la Mbali—Australia. (Tembelea Tovuti ya jw.org/sw, na tafuta kwenye KUTUHUSU > UTENDAJI.) Zungumzia matokeo mazuri kwenye video hiyo ambayo familia hiyo ilipata kwa sababu ya kuhubiri katika eneo la mbali. Mhoji mhubiri yeyote kutanikoni ambaye amewahi kuhubiri katika eneo la mbali. Alipata matokeo gani mazuri katika familia yake, huduma, na hali yake ya kiroho? Ni mipango gani aliyohitaji kufanya? Ikiwa kuna yeyote anayetaka kuhubiri katika eneo la mbali, wazee watafurahia kumpa msaada. Kazia kwamba kuhubiri katika eneo la mbali ni njia nzuri ya kutumia wakati wetu. Ikiwa video hiyo haipatikani, wahoji wahubiri ambao wamewahi kuunga mkono mipango ya kutaniko ya kuhubiri eneo la mbali.
Wimbo mpya 139 na Sala
Kikumbusho: Tafadhali sikilizeni kwanza muziki wa piano, kisha mwimbe wimbo huo mpya.