Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 27, 2015. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
Upendo mshikamanifu ni nini, na kwa nini tunauhitaji maishani? (Rut.1:16, 17) [Mac. 2, w12 7/1 uku. 26 fu. 5]
Kwa nini Ruthu alijulikana kuwa “mwanamke bora sana”? (Rut.3:11) [Mac. 2, w12 10/1 uku. 23 fu. 1]
Mfano wa Hana unawezaje kutusaidia tunapokabili matatizo? (1 Sam. 1:16-18) [Mac. 9, w07 3/15 uku. 16 fu. 4-5]
Mvulana Samweli alipoendelea “kukua akiwa na Yehova,” ni nini kilichomlinda kutokana na mfano mbaya wa wana wa Eli? (1 Sam. 2:21) [Mac. 9, w10 10/1 uku. 16 fu. 3-4]
Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Sauli wa kutotenda bila kufikiri “watu wasiofaa kitu” walipokataa utawala wake? (1 Sam. 10:22, 27) [Mac. 23, w05 3/15 uku. 23 fu. 1]
Kwa nini Sauli alikosea sana kufikiri kwamba dhabihu ni bora kuliko kumtii Yehova? (1 Sam. 15:22, 23) [Mac. 30, w07 6/15 uku. 26 fu. 3-4]
Kwa nini inatia moyo kujua kwamba Yehova ‘huona jinsi moyo wa mtu ulivyo? (1 Sam. 16:7) [Apr. 6, w10 3/1 uku. 23 fu. 7]
Kulingana na Methali 1:4, tuna uwezo gani ambao Yehova anataka tuutumie tunapokabili hali ngumu? (1 Sam. 21:12, 13) [Apr. 13, w05 3/15 uku. 24 fu. 4]
Kwa nini tunaweza kusema kwamba Abigaili hakuasi ukichwa wa mume wake alipompa Daudi na wanaume wake chakula? (1 Sam. 25:10, 11, 18, 19) [Apr. 20, w09 7/1 uku. 20 fu. 3]
Abigaili aliomba msamaha kwa kosa ambalo hakufanya. Tunanufaikaje kutokana na mfano wake? (1 Sam. 25:24) [Apr. 20, w02 11/1 uku. 5 fu. 1, 4]