Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 27
JUMA LINALOANZA APRILI 27
Wimbo 1 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 23 ¶19-23, sanduku kwenye uku. 239 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 26-31 (Dak. 8)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Tembeeni kama watu wenye hekima kwa ‘kujinunulia wakati unaofaa.’—Efe. 5:15, 16.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko. Unaweza kuzungumzia kuhusu hali ya Jumba la Ufalme. Bango la Jumba la Ufalme linapaswa kuwa nadhifu na safi na liandikwe saa za mikutano. Wapongeze wahubiri kwa kutunza Jumba la Ufalme na mazingira yake. Mazungumzo yategemee 1 Pet. 1:16 na kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 121-122.
Dak. 15: “Funua Nguvu za Neno la Mungu Katika Huduma Yako.” Mazungumzo. Halafu, panga kuwe na onyesho fupi lenye sehemu mbili. Kwanza, mhubiri anamtolea mwenye nyumba broshua Habari Njema kwa kunukuu 2 Timotheo 3:16, 17, bila kufungua Biblia. Kisha, mhubiri huyohuyo anafanya onyesho hilo tena, lakini wakati huu anasoma andiko hilo moja kwa moja kwenye Biblia. Waombe wahubiri waeleze kwa nini sehemu ya pili ya onyesho hilo inaweza kuwa na matokeo mazuri zaidi.
Wimbo 124 na Sala