Matangazo
◼ Januari 2006: Kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991, kinaweza kutolewa. Makutaniko yasiyo na vitabu hivyo vya zamani akibani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, ikiwa kinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo hayana kitabu hiki yanaweza kutoa kitabu kingine cha zamani kinachopatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Machi: Tutatoa kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu waliopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutawatolea hasa kile kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tunapaswa kuwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia tukitumia kitabu hicho.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Aprili una miisho-juma mitano, huo ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 5, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Unaweza Kuishi Maisha Yenye Amani Sasa—Na Milele!”
◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango inayofaa ya kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu siku ya Jumatano, Aprili 12, baada ya jua kushuka. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, mkate na divai hazipaswi kupitishwa kabla ya jua kushuka. Chunguzeni wakati ambapo jua litashuka katika eneo lenu siku hiyo. Ni afadhali kila kutaniko liadhimishe Ukumbusho likiwa peke yake. Hata hivyo, huenda hilo lisiwezekane. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, kutaniko moja linaweza kutumia Jumba la Ufalme na yale mengine yanaweza kukutanika mahali pengine jioni hiyo. Ikiwa makutaniko kadhaa yatatumia jumba moja, tunapendekeza kuwe na muda wa angalau dakika 40 kati ya programu ili wote wafaidike kikamili na pindi hiyo. Hakikisheni kwamba hakuna msongamano wa magari. Pia, hakikisheni kuna mahali pa kuegesha magari na pa kushusha na kubeba abiria. Mabaraza ya wazee yanapaswa kufanya mipango inayofaa.
◼ Iwapo utapanga kutembelea nchi nyingine, na utake kujua tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano au kusanyiko, unapaswa kuuliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Kuna orodha ya anwani za ofisi ya tawi katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni.