(1) Swali, (2) Andiko, na (3) Sura
Njia rahisi ya kutoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? ni (1) kumuuliza mwenye nyumba maoni yake kuhusu jambo fulani, (2) kusoma andiko linalohusiana na jambo hilo, kisha (3) kumwonyesha katika kitabu hicho sura inayozungumzia jambo hilo na kusoma maswali ya utangulizi ya sura hiyo. Mwenye nyumba akivutiwa, unaweza kumwonyesha jinsi ya kujifunza Biblia ukitumia mafungu ya kwanza ya sura hiyo. Unaweza kutumia njia hii kuanzisha funzo unapomtembelea mtu mara ya kwanza au unapofanya ziara ya kurudia.
◼ “Je, unafikiri wanadamu wanaweza kumjua Muumba mwenye nguvu zote, kama inavyoonyeshwa katika andiko hili?” Soma Matendo 17:26, 27, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 1.
◼ “Kwa kuwa tuna matatizo mengi leo, je, unafikiri tunaweza kupata faraja na tumaini kama inavyoonyeshwa katika andiko hili?” Soma Waroma 15:4, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 2.
◼ “Ikiwa ungekuwa na uwezo, je, ungekomesha mambo haya?” Soma Ufunuo 21:4, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 3.
◼ “Je, unafikiri watoto wetu watakuja kufurahia hali zinazozungumziwa katika wimbo huu wa zamani za kale?” Soma Zaburi 37:10, 11, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 3.
◼ “Je, unafikiri maneno haya yatakuja kutimizwa?” Soma Isaya 33:24, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 3.
◼ “Umewahi kujiuliza ikiwa wafu wanajua mambo ambayo wale walio hai wanafanya?” Mruhusu ajibu, kisha usome Mhubiri 9:5. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 6.
◼ “Je, unafikiri kwamba siku moja tutawaona tena wapendwa wetu waliokufa, kama Yesu alivyosema katika mistari hii?” Soma Yohana 5:28, 29, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 7.
◼ “Unafikiri ni nini kinachohitajiwa ili mapenzi ya Mungu yatendeke duniani kama mbinguni, kulingana na andiko hili linalojulikana sana?” Soma Mathayo 6:9, 10, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 8.
◼ “Je, unafikiri tunaishi katika nyakati zinazotabiriwa katika unabii huu?” Soma 2 Timotheo 3:1-4, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 9.
◼ “Watu wengi hawaelewi ni kwa nini matatizo ya wanadamu yanazidi kuwa mabaya. Je, umewahi kujiuliza ikiwa matatizo hayo yanazidi kuwa mabaya kwa sababu inayoonyeshwa katika andiko hili?” Soma Ufunuo 12:9, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 10.
◼ “Je, ungependa kupata jibu la swali kama hili?” Soma Ayubu 21:7, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 11.
◼ “Je, unafikiri kwamba kufuata shauri hili la Biblia kutawasaidia watu wawe na familia yenye furaha?” Soma Waefeso 5:33, kisha umruhusu ajibu. Baada ya hapo, zungumzia sura ya 14.
Unaweza kuripoti funzo la Biblia baada ya kuliongoza mara mbili tangu ulipomwonyesha mwenye nyumba jinsi funzo linavyofanywa na ikiwa unafikiri kwamba funzo hilo litaendelea.