Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Je, unafikiri Mungu anajali kuharibiwa kwa mazingira? [Mruhusu ajibu, kisha usome Ufunuo 11:18.] Makala hii inatoa sababu za Kimaandiko za kuwa na matazamio mazuri kuhusu hali ya baadaye ya dunia.” Mwonyeshe makala kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Januari
“Watu wengi hufikiri kwamba wanaadhibiwa na Mungu wanapopatwa na matatizo. Je, umewahi kufikiri hivyo? [Mruhusu ajibu, kisha usome Yakobo 1:13.] Makala hii inaeleza chanzo hasa cha matatizo yetu na kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba matatizo yetu yataisha hivi karibuni.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Je, unafikiri dini zote zinakubaliwa na Mungu? [Mruhusu ajibu.] Ona maoni ya Yesu kuhusu jambo hilo. [Soma Mathayo 15:8, 9.] Makala hii inachunguza ikiwa Mungu anakubali aina zote za ibada.” Mwonyeshe makala kwenye ukurasa wa 9.
Amkeni! Februari
“Vitu vyote vilivyo duniani vinaonyesha kwamba dunia iliumbwa itegemeze uhai. Je, unafikiri hii ilikuwa aksidenti tu, au unaamini ni wonyesho wa kwamba kuna Muumba? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wanakubali maneno ya Andiko hili. [Soma Zaburi 104:24.] Gazeti hili linachunguza uthibitisho wa kisayansi na wa Kimaandiko kwamba kuna Muumba.”