Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 9
JUMA LINALOANZA MACHI 9
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mwanzo 40-42
Na. 1: Mwanzo 40:1-15
Na. 2: Tuepuke Vishawishi (lr sura ya 9)
Na. 3: Jihadhari na Roho ya Kujitegemea!
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo. Waombe wasikilizaji waeleze jambo moja au mambo mawili yaliyoonwa kuhusu utangulizi waliotumia walipowaachia watu magazeti na matokeo waliyopata.
Dak. 15: Watu Wengine Wanapotaka Majibu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kichwa kidogo kinachoanzia kwenye ukurasa wa 177 wa kitabu Shule ya Huduma. Onyesha jinsi mhubiri anavyoweza kumjibu mfanyakazi au mwanashule mwenzake anayeuliza swali kuhusu imani yetu. Mhubiri huyo anajibu kwa utulivu na kwa “tabia-pole na heshima kubwa.”—1 Pet. 3:15.
Dak. 15: “Jitayarishe Kikamili kwa Ajili ya Ukumbusho.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza mipango ya kutaniko lenu kwa ajili ya Ukumbusho.