Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Kwa kuwa rasilimali za dunia zinatumiwa vibaya, je, unafikiri dunia itaokoka? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kufariji. [Soma Zaburi 104:5.] Makala hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wakati ujao ya dunia.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Amkeni! Apr.
“Kwa kuwa tuna shughuli nyingi, watu wengi wanashindwa kupanga wakati wao ili wapate nafasi ya kumwabudu Mungu. Je, unaona hilo kuwa jambo gumu? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Waefeso 5:15-17.] Makala hii inaonyesha maelezo yenye usawaziko ya Biblia kuhusu kiasi cha wakati na nguvu ambacho Mungu anataka tutumie katika utumishi wake.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Watu wengi wanasema kwamba wanaamini mambo ambayo wanaweza kuona tu. Je, unakubaliana nao? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Waroma 1:20.] Gazeti hili linazungumzia sifa tatu za Mungu ambazo tunaweza kuona waziwazi katika uumbaji na linazungumzia jinsi kujua sifa hizo kunavyopasa kutuchochea.”
Amkeni! Mei
“Watu wengi leo wanaogopa wakati ujao. Je, unafikiri mambo yatakuwa bora zaidi, au yatakuwa mabaya zaidi? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba hivi karibuni Mungu atatatua matatizo mazito ambayo wanadamu wameshindwa kutatua.”