Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara Wa Mlinzi Mac. 15
“Mara nyingi watu huzungumzia kurudi kwa Yesu Kristo. Je, unafikiri tunapaswa kulitarajia tukio hilo kwa hamu au tunapaswa kuliogopa? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi mwandishi wa Biblia Yohana alivyohisi kuhusu tukio hilo. [Soma Ufunuo 22:20.] Gazeti hili linaelezea kile ambacho kurudi kwa Kristo kutatimiza.”
Amkeni! Mac.
“Viongozi wengi duniani ni wenye kiburi. Je unadhani kwamba mtazamo huo huchangia amani na muungano duniani? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyosema kuhusu kiburi. [Soma Methali 16:18.] Makala hii inaonyesha umuhimu wa kuwa mnyenyekevu.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 20.
Mnara Wa Mlinzi Apr. 1
“Karibu kila siku tunahangaikia afya yetu, familia zetu, na kazi yetu. Unafikiri tunaweza kupata wapi majibu yenye kutegemeka na yanayofaa kuhusu mambo hayo? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inasema kwenye 2 Timotheo 3:16. [Soma.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia katika njia nyingi mbalimbali.”
Amkeni! Apr.
“Katika sehemu nyingi ulimwenguni, watu wanahisi kwamba viwango vya maadili vimeporomoka. Je, wewe umeona jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Hali tunazoziona leo zinatimiza unabii wa Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:2-4.] Gazeti hili linaelezea mporomoko huo wa maadili unamaanisha nini na unaipeleka wapi jamii.”