Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Kila siku tunasikia habari kuhusu mateso, magonjwa, na kifo. Je, umewahi kujiuliza ikiwa tutaokolewa kutoka katika shida hizo zote? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili la Biblia limewapa mamilioni ya watu tumaini. [Soma Yohana 3:16.] Gazeti hili linazungumzia kichwa, ‘Jinsi Kifo cha Yesu Kinavyoweza Kukuokoa.’”
Amkeni! Mac.
“Je, unafikiri ushirikina una madhara, au si hatari? [Mruhusu ajibu.] Biblia inasema jambo fulani lenye kupendeza. [Soma Isaya 65:11.] Makala hii inaonyesha ikiwa kuna upatano kati ya ushirikina na mafundisho ya Biblia.” Zungumzia makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Je, hungependa kuona unabii huu ukitimia? [Soma Isaya 2:4. Kisha umruhusu ajibu.] Ona kwamba Mungu ataingilia mambo ya wanadamu na ‘kunyoosha mambo.’ Biblia inasema kwamba Mungu atapigana vita vinavyoitwa Har–Magedoni ambavyo vitakomesha vita vyote. Gazeti hili linaeleza Har–Magedoni ni nini na kwa nini tunapaswa kuitazamia kwa hamu.”
Amkeni! Apr.
“Je, unafikiri kwamba huenda tunaishi katika kipindi kinachofafanuliwa hapa? [Soma 2 Timotheo 3:1-4. Kisha umruhusu ajibu.] Kuna sababu nzuri ya kuchunguza kwa makini siku hizi za mwisho kwa sababu kuwapo kwa siku za mwisho kunaonyesha kwamba hivi karibuni mambo yatakuwa mazuri duniani. Gazeti hili linaeleza habari hiyo.”