Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Je, unafikiri kwamba leo kuna habari nyingi kupita kiasi? [Ngojea jibu.] Hata hivyo, hakuna habari muhimu zaidi kuliko ile inayopatikana katika mstari huu. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza maana ya ‘uzima wa milele’ na jinsi tunavyoweza kupata ujuzi unaoongoza kwenye uzima huo.”
Amkeni! Apr. 22
“Ingawa huenda Yesu Kristo ndiye mtu anayejulikana zaidi aliyepata kuishi, watu wengi wangetaka kumfahamu vizuri. Je, unajua kwamba hata wafuasi wake mwenyewe hawakumfahamu vizuri? [Ngojea jibu, kisha usome Marko 4:41.] Gazeti hili linaeleza kile ambacho Biblia inasema kuhusu utambulisho kamili wa Yesu.”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Wakati mpendwa anapokufa, tunatamani kumwona tena, sivyo? [Ngojea jibu.] Watu wengi wamepata faraja kupitia ahadi ya ufufuo inayopatikana katika Biblia. [Soma Yohana 5:28, 29.] Gazeti hili linazungumzia wakati ambapo ufufuo utatukia na wale watakaofufuliwa.”
Amkeni! Mei 8
“Wazazi wengi huwachagulia watoto wao sinema watakazotazama. Je, umeona kuwa ni vigumu kupata sinema zinazofaa kwa ajili ya familia yako? [Ngojea jibu, kisha usome Waefeso 4:17.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwasaidia watoto wao wachague sinema zinazofaa.”