Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Je, unafikiri hali ingekuwa bora duniani kama watu wote wangefuata kanuni hii ya Biblia? [Soma Waroma 12:18, kisha ungoje ajibu.] Ikiwa ndivyo, umewahi kujiuliza kwa nini Mungu aliwaamuru watu wake wa kale wapigane vita na maadui wao? Makala hii inazungumzia jibu la Biblia.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 13.
Amkeni! Januari
Soma Matendo 17:31a, kisha useme: “Wengi wanaogopa wanaposikia Siku ya Hukumu ikitajwa. Maoni yako ni nini kuihusu? [Mruhusu ajibu.] Biblia inafundisha kwamba watu watapata baraka nyingi duniani wakati wa Siku ya Hukumu. Makala hii inazungumzia jambo hilo.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Watu wengi wanaamini kwamba wataenda mbinguni watakapokufa. Je, tumaini hilo linakupendeza? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili la Biblia linataja thawabu ambayo watu wengi wema watapata. [Soma Zaburi 37:29.] Gazeti hili linazungumzia mambo ambayo Biblia inasema kuwahusu watu watakaoenda mbinguni na mambo ambayo watafanya humo.”
Amkeni! Februari
“Watu wengi wanatalikiana siku hizi. Je, unafikiri kwamba kila mtu ambaye ameamua kumtaliki mwenzi wake wa ndoa amefikiria mambo yote yanayohusika? [Mruhusu ajibu, kisha usome Methali 14:15.] Gazeti hili linazungumzia mambo manne ambayo watu waliofunga ndoa wanapaswa kufikiria kabla ya kuamua kutalikiana.”