Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Wengi wetu hatuna uhakika kuhusu mambo ambayo tunaweza kumwambia rafiki anayeugua sana au aliye na ugonjwa usioweza kutibika. Una maoni gani kuhusu shauri hili? [Soma Yakobo 1:19, kisha umruhusu ajibu.] Makala hii ina madokezo kadhaa yanayotegemea kanuni za Biblia.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Amkeni! Julai
“Je, wanawake wanapaswa kuwa wahudumu? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inasema kuhusu mwanamke mmoja. [Soma Waroma 16:1.] Hata hivyo, mstari mwingine unasema kuwa wanawake kutanikoni wanapaswa kunyamaza. Kwa hiyo, maoni ya Biblia ni yapi? Makala hii inaeleza kuhusu jambo hilo.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Watu wengi wana wasiwasi kuwa dunia itaharibiwa au kuangamizwa na vita vya nyuklia au mabadiliko ya hali ya hewa. Je, unafikiri jambo hilo litawahi kutokea? [Mruhusu ajibu.] Ona kile Biblia inachosema kuhusu jambo hilo. [Soma Ufunuo 11:18.] Gazeti hili linajibu maswali manne ambayo watu wengi hujiuliza kuhusu mwisho wa dunia.”
Amkeni! Agosti
“Huenda mashahidi wa Yehova wamewahi kuzungumza na wewe. Je, umewahi kujiuliza kwa nini sisi huenda mlango baada ya mlango, hata kama watu wengi hawapendezwi? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 24:14.] Tunatambua kuwa watu wengi wana habari zisizo za kweli kutuhusu. Gazeti hili linaeleza Mashahidi wa Yehova ni akina nani.”