Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Machi 1
Soma Kutoka 20:15, kisha useme: “Ingawa watu wengi wanajitahidi kutii amri hii, baadhi yao wanaamini kwamba mtu hapaswi kulaumiwa akiiba au kudanganya anapokabili hali mbaya sana. Maoni yako ni nini? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia manufaa ya kuwa mnyofu, hata hali iweje.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Amkeni! Machi
“Watu wengi wanaiheshimu Biblia lakini wanaonelea kwamba habari nyingi za Biblia hazina manufaa sana katika ulimwengu wa leo. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu, kisha usome Waroma 15:4.] Makala hii inaonyesha kwamba hata sehemu za kale za Biblia bado ni muhimu.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinze Aprili 1
“Watu wanapoombwa kumtaja mtu mashuhuri zaidi aliyewahi kuishi, wengi wao humtaja Yesu. Je, wewe pia ungemtaja Yesu? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili linaonyesha umuhimu wa kuchunguza maoni yasiyopatana kumhusu Yesu ili tujue ukweli. [Soma Yohana 17:3.] Toleo hili la pekee la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mambo ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu na mafundisho yake.”
Amkeni! Aprili
“Inaonekana kwamba hatuna wakati wa kutosha wa kufanya yote tunayotaka, sivyo? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wamesaidiwa kwa kufuata ushauri huu. [Soma Wafilipi 1:10.] Gazeti hili linatoa mapendekezo ya jinsi tunavyoweza kutumia wakati wetu vizuri.”