Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Machi 1
“Kuna maoni yanayotofautiana kumhusu Yesu. Je, wewe humwona kuwa mwana wa Mungu au mtu mwema tu?” Mruhusu ajibu, kisha msome pamoja habari zilizo chini ya mojawapo ya maswali yaliyoandikwa kwa herufi nzito katika ukurasa wa 16-17, na pia mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Amkeni! Machi
Unapokutana na kijana, mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 26. Kazia fikira kwenye kichwa kidogo cha kwanza na umuulize, “Unafikiri taarifa hizi ni za kweli au si za kweli? [Mruhusu ajibu, kisha usome 2 Wakorintho 7:1.] Makala hii inazungumzia mambo unayohitaji kujua kuhusu kuvuta sigara, kutia ndani jinsi unavyoweza kuacha zoea hilo.”
Mnara wa Mlinzi Aprili 1
“Watu wengi wana imani na maoni tofauti-tofauti kumhusu Yesu. Unafikiri ni muhimu kujua ukweli kumhusu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza mambo ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu—mahali alikotoka, jinsi alivyoishi, na sababu ya kifo chake.”
Amkeni! Aprili
“Je, unakubaliana nami kwamba kumpoteza mpendwa katika kifo ni mojawapo ya hali ngumu zaidi ambayo mtu anaweza kukabili? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wamefaidika na shauri hili. [Soma Zaburi 55:22.] Gazeti hili linazungumzia njia kadhaa za kukabiliana na huzuni, kutia ndani jinsi tunavyoweza kumtupia Mungu mizigo yetu.”