Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Wahubiri wanapaswa kuwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia wanapomwachia mtu kitabu Biblia Inafundisha au ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki nyumbani. Aprili na Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kama vile wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo linapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki, wahubiri wanaweza kutoa kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
◼ Wahubiri wanapaswa kupewa matoleo mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara yanapofika. Hivyo, watapata nafasi ya kuyasoma kabla ya kuanza kuyatumia katika huduma ya shambani.
◼ Ukumbusho utafanywa Jumanne, Machi 30, 2010. Nyimbo zitakazoimbwa kwenye Ukumbusho ni nambari 8 na 109 katika kitabu kipya cha nyimbo. Iwapo kutaniko lenu hufanya mkutano siku ya Jumanne, inafaa kupanga mkutano huo ufanywe siku nyingine katika juma hilo. Iwapo makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile na haiwezekani kufanya mkutano siku nyingine, mkutano huo unaweza kufutwa. Sehemu za Mkutano wa Utumishi zinazohusu sana kutaniko lenu zinaweza kushughulikiwa katika Mkutano wa Utumishi wa juma lingine.