Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Ulimwengu ungekuwa tofauti kwa njia gani kama watu wote wangefuata maneno haya ya Yesu? [Soma Mathayo 7:12, kisha umruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia baadhi ya mafundisho ya Yesu ili kuonyesha mambo ambayo Mkristo wa kweli anapaswa kufanya.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mei
“Je, unafikiri kwamba hali ya uchumi itakuwa bora hivi karibuni? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi hawajui jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia katika nyakati hizi ngumu. [Soma andiko moja linalotajwa katika makala.] Makala hii inaonyesha jinsi ushauri wa Biblia unavyoweza kutusaidia kukabili hali ngumu za uchumi.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Tofauti na vile ilivyokuwa katika miaka iliyopita, dhambi haizungumziwi makanisani siku hizi. Je, unafikiri tunapaswa kulichukua kwa uzito fundisho kuhusu dhambi, au halina maana tena? [Mruhusu ajibu, kisha usome Waroma 5:12.] Gazeti hili linazungumzia maoni ya Biblia kuhusu dhambi.”
Amkeni! Juni
“Yaelekea maisha yanazidi kuwa yenye mfadhaiko siku kwa siku. Unakubaliana nami? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wanaamini kwamba andiko hili linataja jambo moja linalofanya mfadhaiko uzidi siku zetu. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linazungumzia jinsi mfadhaiko unavyotuathiri. Linatoa pia mapendekezo kadhaa kuhusu jinsi ya kuudhibiti mfadhaiko.”