Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Watu wengi wanaamini kwamba watu wote wazuri wataenda mbinguni. Je unaamini hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona vile Biblia inavyosema kuhusu dunia. [Soma Zaburi 37:11, 29.] Makala hii inazungumzia mafundisho ya Yesu kuhusu wakati ujao wa wanadamu hapa duniani.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 22.
Amkeni! Agosti
“Kifo cha mzazi ni jambo lenye kuhuzunisha sana, sivyo? [Mruhusu ajibu.] Wengi wamefarijika kwa kusoma andiko hili la Biblia. [Soma Ufunuo 21:4.] Makala hii inaeleza jinsi mtu ambaye amefiwa na mzazi, na hasa kijana, anavyoweza kufanya wakati hisia kali za huzuni zinapomlemea.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
“Watu fulani wanasema kwamba Mungu anambariki mtu mwaminifu kwa utajiri, lakini umaskini ni ishara ya kwamba mtu hajakubalika mbele za Mungu. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Ona kwamba Yesu hakuwa tajiri. [Soma Luka 9:58.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Mungu anavyowabariki watumishi wake.”
Amkeni! Septemba
“Je, unafikiri kwamba vijana leo wana matatizo mengi kuliko miaka iliyopita? [Mruhusu ajibu.] Wengi wameona kwamba andiko hili linafafanua kinaganaga hali zilizopo leo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linaonyesha mashauri ya Biblia kuhusu mambo ambayo wazazi na vijana wanaweza kufanya wanapokabili matatizo.”