Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Je, unafikiri inawezekana kupata amani ya akili nyakati hizi zenye taabu? [Mruhusu ajibu.] Ona Biblia inavyosema kwenye Wafilipi 4:6, 7. [Soma.] Makala hii inaeleza jinsi tunavyoweza kupata amani kutoka kwa Mungu.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Amkeni! Julai
“Wengi wetu tunashukuru kwa mambo ambayo wazazi wetu wametufundisha. Je, unafikiri ni kukosa heshima kuchunguza mafundisho ya dini tuliyojifunza tulipokuwa watoto? [Mruhusu ajibu, kisha usome 1 Yohana 4:1.] Makala hii inaonyesha kama ni makosa kubadili dini yetu.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Watu fulani husema kwamba dini ni barabara tofauti-tofauti zinazoelekeza watu kwa Mungu yule mmoja. Je, unafikiri kwamba dini zote ni nzuri? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 7:13, 14.] Gazeti hili linataja mambo matatu hususa ambayo Biblia inasema dini nzuri inapaswa kuwachochea watu wafanye.”
Amkeni! Agosti
“Sisi sote tumewahi kubaguliwa kwa njia moja au nyingine. Unafikiri Mungu ana maoni gani kuhusu ubaguzi? [Mruhusu ajibu, kisha usome Matendo 10:34, 35.] Biblia inaweza kutusaidia kuvumilia tunapobaguliwa. Pia inatusaidia kung’oa hisia zozote za ubaguzi ambazo huenda tukawa nazo. Gazeti hili linaeleza jinsi ya kufanya hivyo.”