Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
“Wengi hufikiri kwamba simulizi la kitabu cha Mwanzo kuhusu Adamu na Hawa ni hekaya tu. Wengine wanaamini kwamba Adamu na Hawa walikuwa watu halisi. Unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Ona Yesu alivyosema kuwahusu. [Soma Marko 10:6-9.] Makala hii inathibitisha walikuwa watu halisi, na inaeleza umuhimu wa kuchunguza yale tunayoamini.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Amkeni! Septemba
Soma 1 Yohana 4:8, na useme: “Watu fulani wanaamini kwamba Mungu anawatesa waovu milele motoni. Wengine wanasema wazo hilo halipatani na andiko ambalo tumesoma. Unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha yale Biblia inayofundisha kuhusu jambo hilo.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Sote tunapatwa na matatizo maishani. [Taja matatizo ambayo kwa kawaida yanawapata watu katika eneo lenu.] Je, unafikiri Mungu anaweza kutusaidia kukabiliana na matatizo hayo? [Mruhusu ajibu.] Katika andiko hili Yesu anataja njia moja ambayo Mungu hutusaidia. [Soma Luka 11:13.] Gazeti hili linaeleza roho takatifu ni nini na jinsi inavyoweza kutusaidia.”
Amkeni! Oktoba
“Kila familia hupatwa na matatizo. Unafikiri familia zinaweza kupata wapi mashauri yanayofaa na yenye kutegemeka? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 32:8.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linataja kanuni kadhaa za Biblia, ambazo zikitumiwa, zitasaidia familia.”