Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
“Nyakati nyingine watu hufanya mambo mabaya kwa sababu ya kupotoshwa na dini. Unafikiri ni nini kinachowafanya wadanganywe sana? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inatutia moyo tufanye. [Soma 1 Yohana 4:1.] Makala hii inaeleza kwa nini ni muhimu kulinganisha mambo tunayoamini na yale ambayo Neno la Mungu linasema.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Amkeni! Septemba
Soma Mathayo 5:39, kisha useme: “Unafikiri Yesu alimaanisha kwamba tunapaswa kukaa kimya tunapotendwa vibaya? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu kujilinda na kutafuta msaada wa kisheria.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Ulimwenguni pote, watu wa dini zote husali. Je, unafikiri Mungu husikiliza na kujibu sala? [Mruhusu ajibu.] Biblia hututia moyo tusali. [Soma Wafilipi 4:6, 7.] Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia kuhusu maswali saba ambayo mara nyingi watu huuliza kuhusu sala.”
Amkeni! Oktoba
“Mara nyingi tunasikia kuhusu watu wanaosalitiwa na wenzi wao wa ndoa, wanasiasa, na wengineo. Unaonaje, inazidi kuwa vigumu kupata watu wenye kuaminika? [Mruhusu ajibu.] Wengi wanahisi kwamba andiko hili linatimizwa. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linaonyesha mahali ambapo bado watu wenye kuaminika wanaweza kupatikana.”