Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana trakti hiyo, mhubiri anapaswa kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho, wahubiri wanaweza kumwachia kitabu Mwabudu Mungu, au Ujuzi, au kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995. Broshua Anataka inaweza kutolewa pia. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kinaweza kutolewa. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho, basi mtolee kitabu Ujuzi, Mwabudu Mungu, broshua Anataka, au kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995.
◼ Ratiba ya kila mwaka ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi haitawekwa tena kama nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme. Badala yake, kila kutaniko litapokea nakala mbili za ratiba hiyo. Nakala moja itawekwa kwenye ubao wa matangazo katika Jumba la Ufalme. Nayo ile nyingine itakabidhiwa mwangalizi wa shule kwa ajili ya kupanga migawo ya shule. Wahubiri wataendelea kupokea nakala zao binafsi za Huduma Yetu ya Ufalme ya kila mwezi, na itakuwa na ratiba ya kila juma ya Funzo la Biblia la Kutaniko, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, na Mkutano wa Utumishi.
◼ Kuanzia juma la Machi 1, 2010, kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’ kitatumiwa kwa ajili ya Funzo la Biblia la Kutaniko. Makutaniko yanayohitaji vitabu hivi, yanapaswa kuviagiza katika agizo lao linalofuata.